Serikali yaondoa VAT kwenye taulo za kike
Muktasari:
Bunge lililipuka kwa shangwe na vigelegele
Dodoma. Serikali imefuta Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), kwa taulo za kike (pedi) zinazoagizwa kutoka nje ya nchi.
Msamaha huo umetangazwa leo Alhamisi Juni 14 na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipokuwa akiwasilisha bajeti kuu ya serikali kwa mwaka 2018/19. “Napendekeza kusamehe VAT kwenye taulo za kike kwa lengo la kuwezesha upatikanaji wa bidhaa hizo kwa bei nafuu kulinda afya ya mama na mtoto wa kike hasa walio vijijini na shuleni,” amesema waziri.
Baada ya kutangaza msamaha huo, Bunge lililipuka kwa shangwe na vigelegele ikizingatiwa ni suala lililokuwa na mchango mkubwa wakati wa mijadala ya hoja za wizara mbalimbali zilizwasilishwa kwenye vikao vinavyoendelea. Hali hiyo ilimfanya pia, Spika Job Ndugai kumuomba Waziri Mpango arudie kipande hicho na akarudia.
Endelea kutufuatilia