Mbunge adaiwa cheti cha ndoa hotelini
Muktasari:
Hoteli hiyo imeweka masharti kwamba mwanamume na mwanamke hawawezi kuruhusiwa kuingia chumba kimoja ikiwa hawajaoana.
Kericho,Kenya.Mbunge wa jimbo la Laikipia nchini Kenya amelalamika kuzuiwa kuingia hotelini yeye na mume wake baada ya kukosa cheti cha ndoa.
Mbunge huyo Catherine Waruguru anasema haki zake za kimsingi zimekiukwa na kutishia kuishtaki hoteli hiyo ya mjini Kericho, eneo la Bonde la Ufa akisema alidhalilishwa.
Hoteli hiyo imeweka masharti kwamba mwanamume na mwanamke hawawezi kuruhusiwa kuingia chumba kimoja ikiwa hawajaoana.
Lakini mbunge huyo anasema wanandoa wengine waliruhusiwa kuingia bila kuulizwa cheti cha ndoa, na kwamba walifanya kila juhudi kuthibitisha kwamba walikuwa mume na mke ingawa hawakuwa na cheti cha ndoa.