
| Yaruhusu waangalizi wa kimataifa | Send to a friend |
| Wednesday, 21 December 2011 13:28 |
|
BARAZA Kuu la Umoja wa Mataifa limelaani ukandamizaji na ukiukaji wa haki za binadamu unaofanywa na serikali ya Syria tangu miezi tisa iliyopita, dhidi ya waandamanaji wanaodai demokrasia. Kura ya baraza hilo inadhihirisha jinsi serikali ya Syria inavyozidi kutengwa katika Umoja wa Mataifa. Hapo awali, Syria ilikubali kuwaruhusu waangalizi wa kimataifa nchini humo na kushirikiana nao kwa ukamilifu. Waangalizi hao wanatazamiwa kwenda Syria mwishoni mwa wiki hii, kusismamia utekelezaji wa makubaliano ya amani ili kumaliza umwagaji damu nchini humo. |
| Last Updated on Wednesday, 21 December 2011 13:29 |















