
| Polisi wauawa wanne wakidaiwa majambazi | Send to a friend |
| Tuesday, 24 January 2012 20:39 |
|
WATU wanne wanaosadikiwa kuwa majambazi wameuwa kwenye pambano na polisi Kijiji cha Nyambula, wilayani Kahama, mkoani hapa wakidaiwa kujiandaa kufanya ujambazi kwa wafanyabiashara eneo la Kakola na mgodi wa Bulyanhulu. Wanadaiwa walikuwa na silaha za kivita na mapanga, walikuwa wakisubiri usafiri wenzao, lakini kabla polisi walipata taarifa kwa raia mwema kuhusu uwapo wa majambazi saba wenye silaha. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Diwani Athuman, alisema majambazi hao waliuawa saa 4:30 usiku na kwamba, baada ya kupata taarifa polisi waliandaa mtego kwa kuwapelekea majambazi hao usafiri eneo walikuwa. Diwani alisema baada ya kufika eneo hilo walikuta ishara ya mfuko wa plastiki uliowekwa jiwe juu yake na majambazi hao waligundua kuwa gari hilo lilikuwa linawasubiri wao, ndipo walipoanza mashambulizi dhidi ya askari ambao nao walianza kujibu mapigo na kuua waane kati ya saba. Hata hivyo, Diwani alisema majambazi watatu walifanikiwa kukimbilia porini na eneo hilo zilipatikana silaha mbili aina ya SMG namba AF364750 na risasi 22 na namba 0801 ikiwa na risasi 25. Risas nyingine 132 zilikutwa kwenye mfuko wa plastiki. Alisema baada ya kupekuliwa walikutwa na simu tatu, fedha za Burundi Faranga 10,000 na Sh2,000. Pia, waliokota kitambulisho cha uraia wa Burundi cha Ndikumana Erick. |
















Comments