MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Kitaifa JK: Tutatumia mkongo kufundishia wanafunzi
BOOKMARK THIS PAGE
JK: Tutatumia mkongo kufundishia wanafunzi  Send to a friend
Thursday, 17 March 2011 20:27

Fredy Azzah
RAIS Jakaya Kikwete, amesema  serikali imebuni mpango maalumu wa kutumia mkongo wa mawasiliano, ili kukabiliana na upungufu wa walimu katika shule za sekondari nchini.Katika kufanikisha  jambo hilo, shule zote za sekondari zitaunganishwa katika mtandao huo ambao utawawezesha mwalimu mmoja kufundisha shule hizo wakati mmoja.

Alisema hayo jana jijini Dar es Salaam alipotembelea Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kukagua utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa Januari mwaka 2006 na kutoa maagizo ya kuboresha elimu kwa miaka mitano ijayo.

"Pamoja na kuwa tuna tatizo la upungufu wa walimu kwa jumla, hali ni mbaya sana kwa walimu wa sayansi, mpaka sasa kuna upungufu wa walimu 34,000 na sisi kwa mwaka uwezo wetu ni kuzalisha walimu 10,000," alisema Rais Kikwete.

Alisema ili kukabiliana na tatizo hilo, serikali itaziunganisha shule za serikali katika mkonga wa taifa wakati ikiendelea pia kuzalisha walimu kadri itakavyoweza."Kutokana na idadi ya walimu wanaosoma, tatizo la walimu litaweza kwisha baada ya miaka mitatu, lakini sasa pamoja na walimu 10,000 kumaliza masomo yao kwa mwaka, unaweza kukuta bado tuna upungufu wa walimu 40,0000 kwa mwaka," alisema

"Tukiziunganisha shule zetu kwenye mkongo wa taifa ambao mpaka kufikia Juni mwaka huu utakuwa umekamilika, mwalimu mmoja akiwa hapa, anaweza kufundisha wanafunzi wa kemia nchi nzima kwa wakati mmoja." alisisitiza.

 Alisema mpango huo ukifanikiwa mwalimu atakaye kuwa yupo kwenye darasa la shule husika, kazi yake itakuwa ni kusimamia wanafunzi kufanya mazoezi na yatakayotolewa na mwalimu aliyekuwa akifundisha kwa njia ya mtandano na kusahihisha kazi zao.

Alieleza kuwa, tayari serikali imeshafanya mazungumzo na kampuni moja ya Kimarekani ambayo itasaidia katika teknolojia hiyo."Wameshanionyesha jinsi tutakavyofanya kwenye maeneo ambayo yana umeme na hata yale yasiyokuwa na umeme," alisema Rais Rais pia aliitaka wizara  kuweka bayana mipango yake kuhusu namna ya kuinua ubora wa elimu.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #26 2011-03-19 07:38
Mh JK anafanyakazi kwa ushabiki na porojo kuliko hali halisi.
Alishabikia sheria ya Uchaguzi kumbe ilikuwa na kasoro nyingi tena za wazi.
Awamu ya nne ni vichekesho vitupu
Quote
 
 
0 #25 2011-03-19 06:41
Huu mpango wa elimu kwa njia ya internet hauhitaji kuwa na elimu ya chuo kikuu kuugundua ni "bluff" nyinginme ya JK kwa watanzania. Inawezekana vipi huu useme kila sekondari itaungunishwa kwa huo mtandao wakati umeme wenyewe hakuna na hata upo unawaka kwa masaa mawili tu kwa siku??
Maabara za kufanyia mazoezi kwa vitendo zipo??
Nina uhakika huu mpango ni ghali sana kuliko kuajiri walimu, na ni mgumu kuutekeleza katika mazingira ya Tanzania bila maandalizi ya muda mrefu.
Vyuo vyetu vikuu havina hata hayo mawasililano ya internet ya uhakika leo Jk anakuja na hadithi ya kuwa na kutumia mkongo wa mawasiliano kufundishia shule za sekondari, huu si Uwe ndawa zimu jamani??
A visonary leader will always set realistic goals, after he has done feasibility studies...hapa mimi naona ni usanii mwingine tena wa serikali ya Jk
Quote
 
 
+1 #24 2011-03-18 22:33
Kuna kipindi nilianza kuamini mwisho wa ahadi zisizotekelezek a wala tija kwa taifa umefika.

Hakuna siku nimekatishwa tamaa lakini nikacheka kama leo kuhusu habari hii. Sijui kama uwezo wa ki-miundo mbinu uko juu kiasi hicho. Na sijui kama mkwere anajua vizuri analolisema. Si vizuri kudharau mamlaka ya juu kiasi hiki lakini mtu unajikuta huna chaguo.

Hahahahahahahhh h!!!
Quote
 
 
0 #23 2011-03-18 19:25
EEMUNGU TUSAIDIE.Kweli Tukiangalia Kwa undani Swala hili Si Tu kufurahi Bali Tutapotea kwa kiwango Gani. Kila Kitu kinahitaji Maandalizi Je Watoto Hawa Wameandaliwa Kwa kiwango Gani Ili kutu mia Mfumo HUU. Kama Tu Wakiwa na mwalimu Hawaelewi. Je Tanzania Elimu Tunaipeleka Wapi Je hiki kizazi Tuakiacha Na urithi gani Kama Matojeo Ya mwaka jana Yalikua Hivyo? Ni Kipindi Amacho Viongozi Wasifurahi Tu Wao kufanikiwa Lakini Tanzania ya kesho Itakua na Watu wa Namna Gani?
Quote
 
 
-1 #22 2011-03-18 18:31
[quote name="wamjinia"]hakuna mwalimu mwenye utaalamu huo anaouzungumzia mheshimiwa mbumbumbu, na wala hakuna wanafunzi wa aina hiyo hapa tanzania wa kuweza kufuatilia mafunzo hayo kupitia mkongo wa taifa..... ]

Did you know that one day you will be in the position to use computer as you do?! What is so special for a teacher to stand before teaching lab and teach! By the way, kama aina hii ya Elimu in question haijawahi na wala haitolewi popote hapa duniani, I can understand. If you please, revisit your statistic.
Quote
 
 
0 #21 2011-03-18 18:04
smart boy? labda boy yule mfanyakazi wa ndani wa nyumba za kihindi lakini huwezi kukubali u[NENO BAYA] kama huu. yaani kiini macho kama hiki mtu unawezaje kukubaliana nacho? hivi anafahamu suala la elimu au anabwabwaja huyu jamaa smart boy sijui smart girl? msitutie hasira maana kuna mambo mengine yanapitiliza hata sio ahadi bali ni kufedheheshana hivi mtu anaesikiliza ahadi za namna hiyo anafikiriaje? mbinu hizo za elimu zinatumika nchi gani na wana maendeleo gani mpaka sasa mpaka watekeleze suala hilo kwanza? hivi tumefikia mahali tumechoka akili mpaka tunatoa ahadi za uongo na uzushi hivyo? nawe unadiriki kusema wakaulizwe wataalamu.... kuna mtaalamu anaesikilizwa hapa tanzania? kwani waziri wa elimu alipotangaza matokeo yeye anahusika na utaalamu wa baraza la mitihani au wizara ya elimu? nchi hii wakati wa kutumia wataalamu na utaalamu bado ni kudanganyana tu kana kwamba hatuelewi kitu ndio maana tunadanganyika kwamba tusipoichagua ccm basi nchi itakuwa na vita....... hatuna rais mwerevu hata kidogo uzeee unamjia vibaya mkwere!
Quote
 
 
+1 #20 2011-03-18 17:51
hizi ni hadithi za abunuwasi, yaani kiongozi wa nchi anapofikia hatua ya kusema uongo kiasi kikubwa kama hiki inasikitisha sana kwa kweli. hivi hata familia yake yaani wake na watoto wanajisikiaje kusikia kauli za kizushi kama hizi kutoka kwa baba wa familia? yaani ni jambo ambalo kwa tanzania ya leo hii halitekelezeki hata kidogo ni ndoto za mchana kuhusu kufundisha kwa kutumia mkongo...... si kwa tanzania nzima hata kwa manispaa moja ya jiji la dar es salaam haiwezekani. hakuna mwalimu mwenye utaalamu huo anaouzungumzia mheshimiwa mbumbumbu, na wala hakuna wanafunzi wa aina hiyo hapa tanzania wa kuweza kufuatilia mafunzo hayo kupitia mkongo wa taifa..... elimu hiyo sijui inatolewa wapi labda kuzimu wanapofuata utajiri na uongozi lakini si tanzania.....
Quote
 
 
+1 #19 2011-03-18 15:33
Mipango ya serikali ya CCM kama ifuatavyo:-
1) Pikipiki (Bajaj ambulance) kwa wajawazito na wagonjwa
2) Elimu Mkongo kwa shule zote za sekondari
3) Kununua/kukodi mitambo ya DOWANS kupunguza makali ya umeme
4) Kuzuia maandamano sababu yanaleta umasikini na kuzidisha uhalifu
5)Mawaziri na watendaji wakuu wa Serikali kupingana hadharani
Kama hii ndio miundombinu, Kweli tumeliwa!!!!!!! !
Quote
 
 
+2 #18 2011-03-18 14:04
siamini kuwa huo mkonga wa mawasiliano ni jibu la tatizo la Elimu ya kiwango cha chini inayotolewa katika miaka karibu 20 hivisasa. mimi nina mapendekezo:
1. Wawekeni walimu wenye uzoefu watengeneze syllabus yenye kuendana na dunia ya millenia ya tatu.
2. Ongezeni mishahara ya walimu. Hiyo mishahara mikubwa wanayopewa wabunge, mawaziri na watendaji wa serikali, ipunguzwe na walimmu waongezewe mishahara yao na kuondolewa kero mbali mbali. Hao wabunge, mawaziri au watendaji bila ya kupata walimu wasingelikuwa katika nafasi walizonazo leo hii na kupata mafanikio waliyo nayo. walimu waongezewe hali bora ya mishahara. Walimu wakipata motisha watafundisha kwa bidii, hawatahangaika kukatikza masomo kwa ajili ya kwenda kujitafutia njia nyingine za mapato, watakuwa na muda wa kutosha kuwafuatilia wanafunzi. Kama mwalimu kwenda kupokea vijisenti vya mshahara wake anazungushwazun gushwa mara huku mara kule, atapata muda gani wa kufundisha? MISHAHARA YA SASA YA WALIMU IONGEZWE MARA TATU ZAIDI. Hivyo walimu watapata motisha.
3. Ondoeni siasa katika sekta nyeti. Wizara kama ile ya elimu, ya afya, ya ujenzi au fedha, inahitaji watendaji wake wakuu kuanzia mawaziri wake kuwa watu wenye uzoefu na usanifu na sekta wanayopewa. Kama sekta ya elimu wakipewa watu ambao hawajui matatizo ya shule, ya wanafunzi, kero za walimu, itakuwa vigumu kwake kutoa sera muafaka za kuboresha sekta hiyo na watendaji wake.
4. tatizo la elimu halitatuliki kwa mikonga, kwani kama ni hivyo wanafunzi wanaweza kubaki nyumbani na kujisomea. Njia za kisasa za mawasiliano zinahitajika kufundishwa na kutumika, lakini haziwezi kum- substitute mwalimu hai. ni njia mbadala lakini haziwezi kumtoa nje mwalimu nje ya ulingo wake. Njia hiyo yaweza kutumika katika elimu za juu za vyuo, lakini kwa ngazi ya sekondari, elimu ni pamoja na maisha ya pamoja, ya kuelimishana, ya kujifunza "ELIMU" na kujenga hoja nyoofu... hapa hakuna jinsi: unahitaji mwalimu, dawati na wenzako. siyo internet. Pia nina wasiwasi na njia hiyo kwani inaua sana mawasiliano ya ki-utu kama ilivyo katika nchi zilizoendelea.
5. Pia tumeanzisha vituo vya elimu vingi mno na hata watu binafsi wameanzisha vituo vya elimu vingi, lakini hawakuanzisha SHULE. shule zina misingi yake... walimu wasanii walioandaliwa vizuri, majengo ya kutosha, maabara ya majaribio, maeneo makubwa kwa ajili ya recreational activities, nyenzo na facilities nyingine. Shule nyingi za kata ni vituo vya elimu au madarasa ya tuition lakini hazina hadhi ya shule. utakuta shule ina walimu 5...hata ukiwa na form one tu idadi hiyo haitoshelezi hata kidogo. Tuanzishe shule, na siyo vituo vya elimu
Quote
 
 
0 #17 2011-03-18 12:55
Chemistry itafundishwa bila maabara ya kufanyia mazoezi. Huyo mwalimu wa mkonga atafanyaje bila kuwapo kwenye maabara ya kemia? Ni vizuri tutafakari vizuri mipango tunayopanga na utekelezaji wake kama utatusaidia kufikia malengo- kutoa wanafunzi bora waliobobea kwa vitendo. Syansi uwa inafundishwa kwa theory na mazoezi ya vitendo kwenye maabara. Theory tupu hazitakusaidia.
Quote
 
 
+1 #16 2011-03-18 11:29
Jk anachekesha kweli. Anazungumzia shule kufundishwa wakiunganishwa na mkonga. Jambo hilo ni ndoto ya mchana. Katika nchi ambako hata maofisini kompyuta zinatumika kwa shida kubwa kwa sababu ya ukosefu wa ujuzi, upungufu wa kompyuta, na zaidi sana umeme, unazungumzwa uwezekano wa sekondari zote kuunganishwa kwenye mkongo. Ndiyo, inawezekana kuunganishwa, lakini Jk asifikiri kuwa utatuzi wa upungufu wa walimu utatatuliwa kwa mtindo huo!!
Quote
 
 
+1 #15 2011-03-18 10:51
Elimu ya Tz haitaendelea kwa kuwajaza wastaafu hapo wizarani. Katibu Mkuu, Prof. Dihenga alishastaafu zamani lakini cha kushangaza ktk uteuzi uliopita yeye umemwacha (sababu ni wa nyumbani!). Vitengo vingi vimeshikiliwa na wakurugenzi ambao ni mababu na mabibi ambao aidha wamestaafu au bado mwaka 1 au 2...hawana hamasa yoyote ya utendaji!
Quote
 
 
+3 #14 2011-03-18 10:49
Kuna mtu ali"define" Kicha..a kwa njia hii na namnukuu...
"Mtu anayefanya jambo lilelile kwa njia ileile akitegemea mabadiliko" sasa kutokana na kufeli mwaka jana je nini tofauti kimefanyika ili mwaka huu uwe tofauti? au tutegemee mtihani rahisi kupita kiasi ili kila aliyeko kidato cha nne mwaka huu afaulu? TANZANIA kazi tunayo..
Quote
 
 
+3 #13 2011-03-18 10:44
Barabara za angani zitajengwa kuanzia 2011! Hivi huyu bado anatufanya sisi [NENO BAYA]? Kompyuta bila umeme...Mbona vyuo vikuu kama UD, SUA na Mzumbe bandwidth bado ni ndogo mno kutosha kuangalia video kiasi cha kufundishia? Shule za kata tulizojenga wenyewe hazina hata madawati - kompyuta mtaziweza?
Quote
 
 
+4 #12 2011-03-18 10:22
hivi Tanzania tumefikia hatua hiyo kweli? utaghalimu kiasi gani cha fedha huo mradi?. ningekuwa mfanya kazi wizara ya elimu ninge-jihuzuru moja kwa moja.
maana, rais kanidharau na kuniona sina uwezo hata wakufikiri kwamba hiyo ahadi haitaweza tekelezeka ndani ya mika 200 ijayo. nakubari 80% ya shule za serikali zipo vijijini. Je, umeme ukikatika sehemu anayo fundishia huyo mwalimu?.

Rais Kiwete ni bora kipindi kile ulikaa kimya kabisaaaaa. Acha kuongea na kutoa ahadi kama hizi. kaa tu kimya, unazidisha hasira zangu, na si mimi tu.
ungetoa ahadi ya kuboresha vyuo vya walimu vilivyopo na kujenga vingine vingi ili kuwepo na uwezekano wa kuvuna walimu zaidi ya 10,000 kwa mwaka. hapo ningekuelewa.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner