MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Kitaifa Wanaomuiga Babu wazidi kuongezeka
BOOKMARK THIS PAGE
Wanaomuiga Babu wazidi kuongezeka  Send to a friend
Monday, 04 April 2011 22:08

Tumaini Msowoya, Iringa
WIMBI la waganga wanaomuiga Mchungaji mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) wa Samunge Loliondo, Ambilikile Mwasapile, limezidi kuongezeka  baada ya mganga mwingine mkoani Iringa, kuibuka na kudai kuwa ana tiba ya aina hiyo.

Mganga huyo, ametajitambulisha kuwa ni Antony Mwandulami kutoka katika Kijiji cha Wangama, wilayani Njombe.Mwandulami alidai kuwa amekuwa akitumia mti kama ule unaotumiwa na Mchungaji Mwaisapila, kutibu magonjwa sugu.Alidai kuwa tayari imepita wiki moja tangu aanze kutoa tiba hiyo na kwamba, watu wameanza kujaa nyumbani kwake.

Kwa mujibu wa mganga huyo, tiba yake inagharimu Sh2,000 kulingana na ugonjwa wa mteja wake."Niliangalia kwenye TV, nikagundua kuwa mti anaoutumia babu hata mimi nilikuwa nikiutumia siku nyingi lakini sikuwa napata mafanikio kwa sababu nilikuwa nikichanganya dawa nyingi. Nilipogundua babu anachemsha mti huo tu, nikaiga na sasa nimeona mafanikio," alisema Mwandulami.

Alisema watoto wa chini ya umri wa miaka 14, amekuwa akiwapa dawa hiyo bure na kwamba, yeye hajaoteshwa kama ambavyo wengine wamekuwa wakidai.“Huu mti nilikuwa nikiujua siku nyingi, nilionyeshwa na mizimu isipokuwa tatizo ndo hilo la kutochemsha ukiwa peke yake," alisisitiza.

Wakati mganga huyo akiwa tayari ameanza kutoa tiba hiyo, Mwenyekiti wa Kamati Utendaji ya Chama cha Waganga wa Jadi mkoani Iringa, Pangael Msekwa, aliwataja wananchi kujihadhari na wimbi la waganga wanaojitokeza kutibu magonjwa sugu.Alisema kuna uwezekano kuwa waganga hao wanaomuigiza babu wa Lilondo ni matapeli.



Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #7 2011-04-05 15:43
ni juu ya mgonjwa kuamua. kama wewe ni kondoo utajua pa kwenda. kama wewe ni mbuzi utajua njia yako. lakini kila mtu atavuna atakachopanda
Quote
 
 
0 #6 2011-04-05 14:38
Mmoja ana "Identity" ya uchungaji; mwingine ya Uganga wa Jadi. Hivi ni vitu viwili tofauti kabisa na vinavyopingana. Lakini la msingi na lisiloingilia uhuru wa mtu, ni maamuzi ya mtu mwenyewe kama ni wapi kunakompa imani ya kupona. Dawa ya asili ipo miaka yote. Kwa imani wako waliokwenda kutibiwa nayo na kwa imani wako waliokataa kabisa kutibiwa na dawa ya asili. Uchungaji au uganga wa kienyeji usihalalishe au kushawishi mtu. Mtu aende kwa hiari yake na si kwa kuiga mtu. Wapagani wao maisha yao yote ni huko kwenye asili, kinachotokea ni kuongezeka kwa wapagani.
Quote
 
 
0 #5 2011-04-05 13:31
kazi kwelikweli kila mtu ss atatoa dawa mm nazani hakuna cha babu wala cha bb wote wa sanii tu.
Quote
 
 
0 #4 2011-04-05 10:19
ummm!!!!!!!! Tz kazi ipo.
Quote
 
 
0 #3 2011-04-05 09:31
Si babu wala hao wenzake wote ni Matapeli watupu, BABU anatangazwa na vyombo vya habari na hao wenzake wanajitangaza,

Mwisho wa siku itajulikana tu kwamba wote ni wezi. Wanatumia U[NENO BAYA] wa Watanzania kuwaibia na kuwasahaulisha matatizo yao ya msingi.
Quote
 
 
0 #2 2011-04-05 09:17
mwandulami asituletee za kuletwa hapa,nani asiyemfahamu huyo kwa mauchawi yake mengi na manyoka.mbona watu wengi huenda kwake kupata kinga je hiyo kinga alioteshwa au.MWANDULAMI KWANZA UNAAGUA KWAHIYO WEWE NI TAPELI WA DUNIA NAKUSHAURI UACHANE NA MWAISAPILE.WEWE ENDELEA NA WAFANYABIASHARA WAKO UWAJAZIE BIDHAA MADUKANI NA HATIMAYE WAFE MASKINI KWA SABABU YA MANYOKA YAKO,KWANZA USITAKE TUKUUMBUE HEBU TULIA WATU TUPATE TIME YENYE BARAKA ZA MUNGU SI KAMA YAKO YENYE BARAKA ZA SHETANI MKUU
Quote
 
 
+2 #1 2011-04-05 08:46
watu wasifanye mchezo na maisha ya watu caz sasa ushakua kama mchezo wa kuigiza......km alikua anautumia siku nyingi na amekua anachanganya na midawa yake mingi isiyo tibu, amwache babu afanye kazi ake......!!!!ACHENI UTAPELI......!!!!!
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner