
| Utafiti: Waliopata kikombe cha Babu wengi wamepona | Send to a friend |
| Wednesday, 03 August 2011 22:59 |
|
Leon Bahati Hiyo ni kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Taasisi ya Synovate kuanzia Mei 2 hadi 19, mwaka huu na kuwahoji watu 1,994 wenye umri zaidi ya miaka 18 maeneo mbalimbali nchini.Utafiti huo uliotolewa na Synovate kwa gazeti hili jana, unaeleza kuwa ni asilimia saba waliosema hawakupona wakati asilimia 15 walisema hawajui. “Asilimia 78 ya waliotibiwa kwa kikombe cha Babu wa Loliondo, walisema wamepona magonjwa yaliyokuwa yanawakabili,” inaeleza sehemu ya ripoti hiyo ya utafiti. Utafiti wa Synovate umekuja wakati ambapo utafiti wa awali uliofanywa na serikali juu ya dawa hiyo ya Babu kuinyesha kuwa ina uwezo wa kutibu magonjwa sugu kama vile kisukari, saratani, moyo na Ukimwi. Serikali ilisema bado inaendelea na utafiti zaidi juu ya dawa hiyo, ambao unaweza kuchukua muda wa hadi miaka mitatu ikizingatia kuwachunguza waliotibiwa na kiwango cha dozi, kulingana na aina ya ugonjwa. Asilimia 83 walisema ni vigumu kupata dawa ya mchungaji huyo maarufu kama Kikombe, huku asilimia 17 wakaonyesha hakuna tatizo la kumfikia.Hata hivyo, kati ya waliokwenda asilimia 25 hawakuwa tayari kutaja magonjwa waliyokwenda kutibiwa, wakati asilimia 24 walisema ni kisukari. Magonjwa mengine na asilimia ya watu walioenda kutibiwa kwenye mabano ni moyo (22), Ukimwi (13), saratani (12), vidonda vya tumbo (7), pumu (5), magonjwa ya ngozi (4), maumivu ya miguu (4), kifua kikuu (3), maumivu ya tumbo (3), maumivu ya uti wa mgongo (2), maumivu ya kifua (2), macho (1) na waliokwenda bila tatizo maalumu (3). Mchungaji Masapila alijijenga umaarufu mkubwa kuanzia mwanzoni mwa mwaka huu baada ya watu kutoka sehemu mbalimbali nchini na nchi jirani kujitokeza kwa wingi kupata tiba hiyo. Misururu mirefu ya magari ilijipanga kwenda kwa babu na kufanya watu kutumia hadi siku saba kupanga foleni ya kupata dawa. Pia, utafiti wa Synovate ulizingatia kuwa kulikuwa na waganga wa jadi waliojitokeza kutoa tiba sawa na Masapila, lakini licha ya hali hiyo, asilimia 60 walikiamini Kikombe cha Babu. Wengine waliojitokeza na asilimia za kuaminika kwa watu kwenye mabano ni Dogo Jafferi wa Mbeya (9), Magret maarufu kama Bibi wa Tabora (8), Subira Ali (4), Majimarefu (2), Sinkala wa Mbuyuni (2) na babu wa Moma Mtwara (2). |
















Comments
Duh! ulishaona wapi mtu anajua kuwa kapona kwa kujitazama? KJ unaonesha haujui lolote kuhusiana na mwili wa mwanadamu na maradhi wewe unadhani unalitetea neno la BWANA kumbe unawapoteza watu sasa subiri hasira za bwana zije zikushukie
mie naona weye ni mvivu hata wa kufikiria au unafanya kazi na hao M A bazazi hebu eleza hicho cha msingi ulichokisoma kwa makini? Halafu nani alikuambia kuwa ili kujua kama hicho kikombe kinatibu unahitaji kusoma magazeti itś like 1+1 sasa we subiri na imani za upofu
ANKETA ni mojawapo ya applicable methodologies maalumu zinazotumika....na ni sahihi kabisa...
msiwakatishe watu bure kuhusu hii tiba poa!!Jamani tuzidi kupata kikombe cha babu...viva synovate....viva KIKOMBE CHA LOLIONDO KWA BABU
kumbukeni ideology ya maji kuyeyusha risasi kwenye majimaji war na kinjekitile ngwale
MAABARA YA NINI KAMA MTU ALIKUWA ANAUMWA NA SASA AMEPONA, WHAT KIND OF SCIENTIFIC TEST ARE YOU AFTER?? MBONA WATU WANATUMIA MADAWA YA KISAYANSI NA YET WANAKUFA. ACHA FIKRA MGANDO. BABU YUKO JUU NA KIKOMBE CHAKE
Such kind of researches have no benefit to the public!
wenh=gi waliokufa ni wale ambao walikuwa wamezidiwa sana.mbili wale ambao ni wachawi...usisahau pale babu alikuwa ana tumia nguvu za mungu...kama wewe ni mchawi na unaroga na kuua watu sasa ni kwanini wewe unatakla kupona kama kuua si kitu kibaya ni kwanini wewe mchawi hutaki kufa?/ yale yalikuwa mambo ya kiimani zaidi na tusihukumu sana maana atutahukumiwa tusipoangalia...hakuna mtu ana uhakika ZAIDI KWAMBA NUI NINI HASWA KILIFANYIKA ILA MUNGU SI MWANADAMU MANA YEYE ANAJUA YOTE.