MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Kitaifa Sekondari Dar wazichapa kavukavu, polisi yashikilia 20
BOOKMARK THIS PAGE
Sekondari Dar wazichapa kavukavu, polisi yashikilia 20  Send to a friend
Saturday, 11 September 2010 09:02

Ndeninsia Lisley (RCT) na Tumsifu Sanga

KITUO cha daladala Tuangoma Wilaya ya Temeke jana kiligeuka uwanja wa mapigano baada ya wanafunzi wa Shule tatu za Sekondari tofauti kuamua kuonyeshana umwamba wa kupigana hadi kuumizana.

Wanafunzi hao ambao ni wa vidato tofauti katika shule za Sekondari Mikwambe, Tuangoma, Makongo na Changanyikeni zote za Wilaya ya Temeke walifanya tukio hilo muda mfupi baada ya kupanda katika daladala za kuelekea Tuangoma wakitokea Mikwabe.

Filamu hiyo iliyodumu kwa saa kadhaa ilisababisha wanafunzi 14, kujeruhiwa na kukimbizwa katika hospitali ya Wilaya ya Temeke kwa matibabu zaidi.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, (DCP) Suleiman Kova alisema, uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa wanafunzi hao wana mgogoro wa muda mrefu unaotokana na masuala ya kimapenzi wakituhumiana kuchukuliana wasichana.

Kwa mujibu wa Kamanda Kova, ugomvi huo ulisababishwa na baadhi ya wanafunzi wa shule hizo tatu ambazo zipo karibu.

Alisema taarifa za awali zinaonyesha wanafunzi hao ni watukutu, watoro wa vipindi darasani na muda wote hushinda vichakani bila kuhudhuria vipindi.

Kova alisema ugomvi baina ya wanafunzi hao ulianza wakati wakiwa katika daladala wakitokea Mikwambe kuelekea Tunagoma na kwamba walianza kurushiana maneno na baada ya  muda mfupi walianza kupigana.

Kova alisema wakati vurugu hizo zikiendelea mwalimu Mkuu wa Shule ya Tuangoma alitoa taarifa polisi na muda mfupi baadaye askari walifika katika eneo hilo na kufanikiwa kuwakamata wanafunzi 20 wanaosadikiwa kuwa  chanzo cha vurugu hizo. Majina ya wanafunzi hao, yamehifadhiwa.



Alisema jeshi la polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa kushirikana na Ofisa Elimu wa Wilaya ya Temeke pamoja na viongozi wa shule hizo, wanaendelea na uchunguzi kuhusiana na mgogoro huo.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #9 2010-09-13 09:06
Kwa niaba ya wabongo wote wa Europe and America, napend a kuwaalika watanzania wote popote pale mlipo kuungana na sisi kwenye mtandao mpya wa mawasiliano ujulikanao kama Zwapa! (www.zwapa.com). Huu ni mtandao ambao unawaunganisha wabongo walioko maeneo tofauti duniani na wale walioko nyumbani (Tanzania). Ingawa uneanzishwa hivi karibuni, tunashukuru kwamba watu wengi (including Americans and Europeans) wameshajitokeza na kuanza kuutumia. Unaweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kwa kutafuta "Lumumba" kwenye Zwapa au copy and paste Kwa niaba ya wabongo wote wa Europe and America, napend a kuwaalika watanzania wote popote pale mlipo kuungana na sisi kwenye mtandao mpya wa mawasiliano ujulikanao kama Zwapa! (www.zwapa.com). Huu ni mtandao ambao unawaunganisha wabongo walioko maeneo tofauti duniani na wale walioko nyumbani (Tanzania). Ingawa uneanzishwa hivi karibuni, tunashukuru kwamba watu
wengi (including Americans and Europeans) wameshajitokeza na kuanza kuutumia. Unaweza kuwasiliana na mimi moja kwa moja kwa kutafuta "Lumumba" kwenye Zwapa au copy and paste www.zwapa.com/.../lumumba kwenye browser yako.
Thanks!http://www.zwapa.com/profile/8/lumumba kwenye browser yako. Thanks!
Quote
 
 
0 #8 2010-09-12 20:27
Tanzania tunakwenda kubaya,green Guard wa CCM kupasua wenzao ngeo,Gari la Prof Baregu likapasuliwa na kupondwawanafun zi nao wanachapana badala ya kuandaa makongamano.Kizazi hiki cha tabia mbovu z namna hii nani wa kjulaumiwa?Nilitarajia m/kiti wa CCM kutoa tamko kukemea uchafu huu lakini wapi kimya!police nao kimyaa!Hivi kweli wanafunzi wenye kusoma shule zinazotoa Elimu nzuri wanaweza kufanya uchafu kama huu!Biashara ya unga ndo usiseme vijana wana makundi makubwa yanayojihusisha na ubuyaji wa madawa ya kulevya na hasa maeneo ya KURASINI!Tunakw enda wapi jamani!Hii nchi tutamwachia nani Riziwani Kikwete!! Mhh sipati picha hata kidogo!
Quote
 
 
0 #7 2010-09-12 01:48
Mimi ninafikiri serikali kupitia dola inahitaji kufanya kitu ili kuzuia au kuwafanya wananchi kutojiamulia chochote kinachoweza kumdhuru mtu mwingine. Mambo haya yanatakiwa yakemewe angali mapema na wataothibitika wawafanye wengine wafahamu kuwa kufanya hivyo ni kosa. Leo wanafunzi wanafanya hivyo kesho watu wa mtaa fulani. Wanyonge wataishi vipi?
Quote
 
 
0 #6 2010-09-11 16:59
Nakumbuka Mh.W. Bush rais wa USA enzi hizo alitoa speech yake akifungua mkutano wa wanachama wa UN (Umoja wa Mataifa) ?Oct 2007.Alisema Good Education is to have Access to School,Availabi lity of enough Teachers and Text books.Yaani upatikanaji nafasi ya kwenda shule,pawepo na walimu na vitabu vya kutosha.Sasa sijui kama hivi vigezo viliangaliwa kabla ya kuanzisha hizi Sekondari.Sijui Tz tunakokwenda kielimu,wanaoum ia ni mkulima wa jembe la mkono na mfanyakazi wa kipato cha chini maana mzazi mwenye kipato kizuri hawezi kumwacha mwanae aende hizi sekondari,lakin i kwa mwendo huu bila shaka mbeleni, hii EAC wenzetu majirani zetu ndio wanaokuja kuwa wataalam wetu na tutabaki Ma-day workers tusipobadilika.Wenzetu hawatanii na kitu Elimu,Chonde Chonde Wa-Tz wenzangu tuamke kama tulilala hizo vumbi za kampeni za uchaguzi zituletee matunda mazuri sio kuambulia mafua tu.Tuwabane hawa jamaa tumechoka na ahadi za kujengewa barabara hewani na maji ya masaa 24 wakati mabomba yana kutu za miaka nenda rudi.
Quote
 
 
0 #5 2010-09-11 16:19
Hayo ni matokeo ya SEKONDARI za kata wanafunzi wasipofundishwa darasani kutokana na uhaba wa waalimu hujitafutia shughuli nyingine ya kufanya.Huu mpango wa sekondari za Kata unaangamiza kabisa Elimu Tz.Unajua huezi kuaanzisha sekondari bila kufuata uwiano wa Waalimu walioopo au wanaozalishwa yaani [NENO BAYA]liza chuo kila mwaka.Simlaumu sana aliyetoa wazo la hizi sekondari bila shaka hakupata washauri au alikataa ushauri.Jamani kule kuna watoto waliokuwa na akili sana lakini walipofika 'seko-ndali' (yaani kicheko kirefu kwa wale wa Mbeya)hawa watoto ni mbumbumbu tupu.Walimu waliopo wamechanganyiki wa ni mikwaju/fimbo tupu wanatembeza kwa wanafunzi,sijui tunakiandaa kizazi cha aina gani.USHAURI WA BURE SERIKALI FUNGENI SEKONDARI ZOTE AMBAZO HAZINA WALIMU ZAIDI YA SITA YAANI WENYE UWEZO WA KUFUNDISHA BOTH ARTS& SCIENCE SUBJECTS.KWA WAZAZIMKATAE KUDANGANYWA NA UTITIRI WA SEKONDARI SIO KIPIMO PEKEE CHA KUPIMA KUKUA KWA ELIMU BORA FUATILIENI MAENDELEO YA WATOTO WENU WAULIZENI HAO WAHESHIMIWA WATARAJIWA WAMEFANYA &WATAFANYA NINI NA HIZI SEKONDARI MSILEWE NA KOMONI,KANGALA NA WANZUKI NA POROJO ZAO WATOTO WANAPOTEA HIVYO,WAKUU WA SHULE ZOTE ZA SEKONDARI KAENI NA HAO WAKUBWA ILI KUWASHAURI KUZIFUNGA HIZO SHULE AMBAZO HAZIKIDHI VIWANGO LASIVYO MTAENDELEA KUAIBIKA NA DIVISION ZEROs ZA WANAFUNZI WENU MAANA MWANAFUNZI WAKIFAURU PIA NA WAALIMU WAMEFAURU.
Quote
 
 
0 #4 2010-09-11 15:10
Mhariri wa Gazeti hili la Mwananchi kwa nini unaruhusu watu watumie gazeti lako kwa kuwakashifu viongozi wa nchi kama majani ya mbaazi.
Mtu anaandika na kutaja majina kama anataja kilo ya mchele dukani na bila wasiwasi wowote anasema fulani, fulani na fulani ni mafisadi.
Hebu angalia comments za Said mistari miwili ya mwisho. Kwa mantiki ya Said Rais wa Tanzania ana tabia, hulka na desturi za kike baya zaidi Watanzania sote ni wendawazimu kwa kukubali kwetu kuongozwa na mtu asiyekuwa na akili.
Watanzania wenzangu sisi wenzenu wa huku ng'ambo inatuuma sana tunaposoma comments zenu na kubaini kuwa mnawatukana viongozi wa nchi.
Quote
 
 
0 #3 2010-09-11 12:24
Mambo ya ccm hayo wanajitangazia kwamba wamejenga shule nyingi,shule gani hizo hazina walimu watu wamepelekwa pale kujazwa u[NENO BAYA] tu,kikwete na chama chako achia ngazi huna sifa za kuwa kiongozi wa hii nchi,kwanza umeprove kwamba kabila lako ni watu wa kucheza ngoma tu,leo hii ukifariki hakuna wa kukukumbuka kama mkuu wa nchi,utakumbukw a na familia yako tu na mafisadi wenzako akina Lowasa,Rostam Azizi n.k. Hakuna wa kukukumbuka kama nyerere,moringe sokoine na karume.Saizi yako ni wanawake tu huna lolote na usanii wako wa ki[NENO BAYA] tena unatakiwa ukapimwe akili yako.
Quote
 
 
0 #2 2010-09-11 12:13
usiwekama unakua leo,mbona akili yako nahao watoto kama iko sawa,kwahiyo ulitaka ccm iwafundishe hao wazazi namna yakulea na maadili,wewe kama mzazi unatakiwa kujua wajibu wako unashindwa kujua hatamaendeleo ya mwanao shuleni,unaitwa katika vikao vya shule huendi,ndiyo chanzo cha haya yote,leo hii mzazi unaogopa kumwambia mwanao kuhofia atakasirikasi[N ENO BAYA] huu....We Haji nadhani hata ukishindwa kuelewana na mkeo kuhusu maswala yenu ya chumbani unakimbilia kuilaumu serikali
Quote
 
 
0 #1 2010-09-11 10:01
Huo wote ni utovu wa idhamu unaosababishwa na Serekali kutoshirikana na wazazi na walimu kutoa ripotisahihi za maendeleo ya watoto kila muhula.Zamani
kila baada ya miezi mitatu au minne watoto walikuwa wanapewa taarifa za maendeleo yao kupeleka kwa wazazi.Usanii wa CCM umesababisha elimu na nidhamu ya watoto kushuka sana mashuleni.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner