MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Siasa Gamba lazidi kuitesa CCM,sasa kutumia nguvu kujivua
BOOKMARK THIS PAGE
Gamba lazidi kuitesa CCM,sasa kutumia nguvu kujivua  Send to a friend
Tuesday, 29 November 2011 20:42

Leon Bahati 

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekiri kuwa muda wa kuvuana gamba kwa nguvu tayari umefika, lakini mkakati huo utabidi usubiri hadi Februari au Machi mwakani.  Chama hicho kimeeleza sababu za kuuvutia pumzi mchakato huo kuwa ni kukamilisha mchakato wa uundaji wa Tume ya Udhibiti wa Nidhamu na Maadili ngazi ya Taifa kwa chama hicho, ambayo iko kwenye mchakato wa kuundwa.  

Hayo yalielezwa jana Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama katika mkutano wake na waandishi wa habari ambako pia alisema, mipango ya namna tume hiyo itakavyoendesha shughuli zake, imekamilika na kilichobaki ni upatikanaji wa wajumbe wake 14. 

Kazi inayofanyika kwa sasa, alisema Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM (CC), imekuwa ikiandaa namna ya kupata majina ya watu watakaounda kamati hiyo ambao wanaonekana hawawezi kushawishika katika kupendelea.

Wajumbe hao pia hawapaswi kuwa na nyadhifa nyingine zozote zinazoweza kuingiliana mchakato wa kazi yao.  Alisema vikao vya juu, Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) vitapitisha majina ya kamati hiyo katika vikao vyake vitakavyofanyika kati ya Februari na Machi mwakani.  “Mara baada ya tume hiyo kupitishwa, itaanza kazi yake mara moja,” alisema Mukama kufuatia baadhi ya vyombo vya habari kueleza kuwa CCM imeshindwa kutekeleza uamuzi wake wa kujivua gamba ili kukisafisha dhidi ya kashfa za ufisadi zinazowaandama baadhi ya wanachama wake.  

Dhana ya kujivua gamba ilipitishwa na Nec katika vikao vyake vilivyofanyika kati ya Aprili 10 na 11 mwaka huu kwa kuwataka wale wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi kujiondoa wenyewe kwenye nafasi zao la sivyo chama kingetumia nguvu kuwaondoa.  Akirejea maagizo ya Nec Mukama alisema “Viongozi wa CCM wanaotuhumiwa kwa ufisadi watafakari, wajipime na kuchukua hatua wenyewe kwa maslahi ya chama. Wasipofanya hivyo chama kitawawajibisha mara moja.” 

Akieleza juu ya tathmini ya chama hicho kuhusu kujivua gamba kwa hiari, Mukama alisema; “Hali ilivyo hadi sasa takribani miezi saba ya azimio hili kupitishwa, bado hatujapata mwitikio wa kuridhisha kutoka kwa viongozi wa ngazi yoyote wa chama chetu, ambao ni walengwa.”

 Kwa sababu hiyo, akasema: “Bila shaka wakati sasa umefika kwa chama kutekeleza ile sehemu ya pili ya azimio husika kwa kuwawajibisha wahusika.”  

Kilichokifanya chama hicho tawala kuwa njia panda katika kutekeleza azimio hilo, Mukama anaeleza kwamba ni namna ambayo mpango huo utatekelezwa kwa haki na mtu asionewe.  Alisema utaratibu huo utapaswa kufanyika kwa kutumia kanuni za chama hicho za uongozi na maadili, ambapo tayari NEC na CC wameridhia iundwe Tume mpya itakayofanya kazi hizo.  

Katika ngazi ya Taifa, alisema itaitwa Tume ya Udhibiti wa Nidhamu na Maadili ya Viongozi na ngazi nyingine kuanzia Mkoa, Wilaya na Tawi, zitaitwa kamati za kudhimiti nidhamu na maadili.  Kulingana na mfumo huo mpya, Mukama alisema tume na kamati hizo zitakuwa na madaraka ya kumchukulia hatua za kinidhamu kiongozi yoyote yule katika ngazi husika pasipo haja ya kusubiri utaratibu wa vikao ndani ya chama.  
 
Alisema kazi hiyo itaweza kufanyika baada ya kukamilika kwa mchakato wa kuunda Tume ya Udhibiti wa Nidhamu na Maadili, ambayo mchakato wake unakamilishwa na Secretarieti ya NEC.  Alipoulizwa juu ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya baadhi ya wanachama wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) waliodaiwa kutaka kuasi chama, alikiri kuwa uchunguzi ulifanywa dhidi ya mienendo yao kulingana na malalamiko juu yao.  

Alisema mmoja wa viongozi wa CCM mkoani Mara ndiye aliyewasilisha malalamiko hayo akituhumu kikundi kilichodaiwa kuongozwa na Hussein Bashe.   

Katika uchunguzi huo, Mukama alisema walibaini kuwa kwenye mkutano uliofanywa na Bashe haukuwa na mikakati ya kufanya uasi ndani ya chama ila kulikuwapo na hitilafu zilizojitokeza kutoka kwa watu wachache.  Mukama aliwahakikishia waandishi wa habari kuwa vikao hivyo vya juu vya CCM viliangalia mkanda wa video wa mkutano huo na kujiridhisha kuwa Bashe hakuendesha mambo kinyume na taratibu za chama.

Awali akizungumza na waandishi wa habari  mara baada ya kikao cha NEC kilichofanyika Dodoma juma iliyopita, Mukama alisema kati ya maazimio yaliyotolewa na kikao hicho Aprili mwaka huu, azimio namba 27 “linahitaji kutekelezwa haraka iwezekanvyo.”  “Dhana hiyo ya kukipatia chama chetu sura mpya ndiyo iliyopewa jina la kujivua gamba na sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa

imekwishatengeneza mpango wa utekelezaji wa maamuzi hayo,’’ alisema Mukama.  Alisema katika kikao chake kilichomalizika juzi, NEC imeamua kuwa viongozi wa CCM wanaotuhumiwa kwa ufisadi ndani ya chama walipaswa kujipima na kujitafakari wenyewe na ikibidi wachukue hatua jambo ambalo halijatekelezwa hadi sasa.  ENDS


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #24 2011-11-30 20:49
Toka lini kobe akajivua gamba?
Quote
 
 
0 #23 2011-11-30 20:15
Quoting joseph Masanja:
HUYU MUKAMA ALIKUWA MSAIDIZI WA KINGUNGE NGOMBALE SASA NADHANI AKILI YAKE IMEKUWA HAIFANYI KAZI SAWA SAWA MAANA ALIZOEA KUTUMWA. TUMESEMA CCM IMEACHANA NA DHANA YA KUJIVUA GAMBA YEYE BADO ANALETA LONGOLONGO!

CCM NATAKA IFE MAANA HAINA MAANA YEYOTE ILE
Quote
 
 
0 #22 2011-11-30 20:12
kazi yoyote ni vizuri ikianza iishe na ni isipo isha mantiki ya kufanya hivyo haipo inaweza kuwafanya watu wakose imani na pengine ukose nafasi ya kuwaongoza
Quote
 
 
0 #21 2011-11-30 16:23
una hangaika tu ewe njaa kali,Urais hampati ngo,Muswada umeshasainiwa,U rais 2015 uko palepale,mtaish ia hivyo hivyo kuandamana,kusu sia bunge na kwenda kuuza Sura kwa Rais wetu Ikulu na kupiga nae picha'Quoting maganga wa maganga:
kujivua gamba? ccm inatakiwa kujivua madaraka kwa maana hebu tajeni mafanikio yenu toka uchaguzi mkuu.baadhi ya sehemu nchini hazijawahi kuwa na maji ya bomba eti miaka hamsini ya uhuru what a joke.halafu kuna mropokaji mnamuita katibu mwenezi jamani hebu mpelekeni shule kwanza hana sense wala substance ya vitu anavyoropoka.juzi lowassa kawapandishia kwa hoja na mwenyekiti wenu kahusishwa mbona mmeshindwa kujibu? mukama we kaa kimya huko kutapatapa kwenu wala hamna mtu ana interest. halafu nasikia mnashikana mashati kuhusu uchaguzi wa 2015 jamani watanzania tutakubali kuongozwa tena na wabaishaji hawa? mungu inusuru tanzania amen.
Quote
 
 
+2 #20 2011-11-30 15:07
hayo magamba wiizii mtupu !!!!
Quote
 
 
+2 #19 2011-11-30 13:00
ni dalili za wazi a udhaifu kwa mchakato huu kuendelea kuahirishwa wakati walengwa wake walijulikana na kutajwa hata kwa majina na baadhi yao kujiondoa wenyewe.muda wa mabadilliko ni sasa kuendelea kuahirisha mchakato ni kuwapa walengwa muda wa kujipanga na kuandaa kundi kubwa zaidi la kuwaunga mkono. mfa maji haachi kutaptapa
Quote
 
 
+1 #18 2011-11-30 12:32
Wanasaikologia wanasema ukiona Tangazo lililobandikwa kwenye ubao wa matangazo limachanwa ujue limesomwa,Anach o kisema Mukama ni kweli kimejadiliwa kwa mujibu wa usemi huo hapo juu na uhakika wake unathibitika kwenye utendaji ebu tuwape mda ccm tuone wanacho fanya katika hili ila napenda kutoa rai kwa ccm wajue kila vikao na mambo wanayojadili na sisi wananchi pia tunashiliki kinadhalia na ushiliki huu mtauona live mwaka 2015 katika uchaguzi mkuu... Mungu ibaliki Tnzania,,,Mungu ibaliki Ccm Amina
Quote
 
 
+1 #17 2011-11-30 12:29
Nadhani CCM waacheche papara katika hili. wafanye uchunguzi wa kina. na wahukumu kwa kufuata haki, sheria na katiba ya nchi!! Huwezi kumhukumu mtu kwa hisia ama kwa maneno ya mtaani ama vyombo vya habari; tafuta ushahidi ujiridhishe paispo na shaka kuwa mhusika ana hatia, ndipo umhukumu. kuna watu CCM wanaitwa magamba lakini ni watgu safi,wachapa kazi na hodari katika utumsishi wa umma na ni watu ambao tanzania yetu inawahitaji. Walimwandama mkapa, Sumaye, nk sasa wameacha wanaita watu magamba hii nidhambi na niwashauri watanzania kama kuna mwenye ushahidi aulete.
Quote
 
 
+1 #16 2011-11-30 12:10
Walionzisha dhana ya kujivua gamba, walikosea kwa kwani wlililenga baadhi ya maadui yao kisiasa kiasi kwamba, wao nao wakaamua kujihami, utekelezaji wake ni mgumu na si kweli kwamba wale wanaotajwa tu ndio wachafu lakini wamekuwa victms wa siasa za makundi
Quote
 
 
+1 #15 2011-11-30 11:46
hivi maana ya kujivua gamba ni nini? Na ni nani anayetakiwa kuvuliwa? Nyie endelezeni hii movie mpaka 15 muone kama wananchi hatujawavua gamba wenyewe
Quote
 
 
0 #14 2011-11-30 11:05
HAYOMAGAMGA NI MAGAMBAGANI MBONA NI MAGUMU
Quote
 
 
+1 #13 2011-11-30 10:51
Tunaomba utekelezaji wa Haraka ili Tujenge Nchi yenu,maana Tukisikia Vikao vya NEC,au CC ajenda ni Gamba tu,jamani wana CCM mbona tunapoteza mwelekeo,kanuni za Chama zipo,Kamati za Maadili zipo,mbona hazifanyi kazi na Mwaka sasa umepita Gamba halijavuliwa,Ny erere alipotangaza kukamatwa kwa Wahujumu Uchumi,enzi za TANU ilikuwa ni Masaa 24 tu,mbona wahujumu Uchumi wa leo wanavuliwa Gamba kwa Kubembelezwa,tu nakwenda wapi wana CCM,leo Katibu Mkuu anasema hadi mwakani mwezi wa pili au wa tatu,Ok tunasubiri,ila mkumbuke kadri mnavyozidikuche lewa kuwavua gamba na ndipo Chama kinavyo zidi kupoteza Umaarufu,maana yake ni Mengi sana yanazungumzwa huku Mtaani.Inakuwa kama kesi ya Nyani unampelekea Ngedere,hatoi hukumu ng'oooooooooo.
Quote
 
 
+1 #12 2011-11-30 10:37
Kuunda kamati hadi ngazi ya matawi maana yake kuna haja ya kubadili katiba ya chama na kama tutabadili katiba February kamati haiwezi kuanza kazi maana mpaka uitwe mkutano mkuu wa chama kuidhinisha mabadiliko hayo
Quote
 
 
+1 #11 2011-11-30 10:37
kujivua gamba? ccm inatakiwa kujivua madaraka kwa maana hebu tajeni mafanikio yenu toka uchaguzi mkuu.baadhi ya sehemu nchini hazijawahi kuwa na maji ya bomba eti miaka hamsini ya uhuru what a joke.halafu kuna mropokaji mnamuita katibu mwenezi jamani hebu mpelekeni shule kwanza hana sense wala substance ya vitu anavyoropoka.juzi lowassa kawapandishia kwa hoja na mwenyekiti wenu kahusishwa mbona mmeshindwa kujibu? mukama we kaa kimya huko kutapatapa kwenu wala hamna mtu ana interest. halafu nasikia mnashikana mashati kuhusu uchaguzi wa 2015 jamani watanzania tutakubali kuongozwa tena na wabaishaji hawa? mungu inusuru tanzania amen.
Quote
 
 
+1 #10 2011-11-30 10:23
ccm mnaogopa nini kumvua gamba Lowasa mbona mnakuwa na kigugumizi,jari buni muone halita salia jiwe juu ya jiwe.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner