MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Siasa JK amteua Lubuva kumrithi Makame Nec
BOOKMARK THIS PAGE
JK amteua Lubuva kumrithi Makame Nec  Send to a friend
Thursday, 22 December 2011 20:08

Leon Bahati
 RAIS Jakaya  Kikwete amemteua Jaji Mstaafu Damian Lubuva kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Lewis Makame, ambaye uitumishi wake kwa umma ulimalizika Julai, mwaka huu.

Amemteua pia Julius Mallaba kuwa Mkurugenzi wa NEC ili kuchukua nafasi ya Rajabu Kiravu ambaye naye amestaafu.Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi,  Phillemon Luhanjo Jijini Dar es Salaam jana, ilieleza kwamba walioteuliwa walianza kazi tangu Jumatatu iliyopita.

Katika uteuzi huo, Rais Kikwete alimteua  Jaji Mstaafu Hamid Mahmoud Hamid kuwa Makamu Mwenyekiti wa NEC.

Kabla ya uteuzi wake, Lubuva alikuwa Jaji katika Mahakama ya Rufani Tanzania na baada ya kustaafu aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Maadili ya Viongozi.

Naye Hamid alikuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar kabla ya kustaafu na anachukua nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Jaji Omari Makungu.

Kwa mujibu wa Luhanjo, Jaji Makungu aliwahi pia kuteuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na baadaye akateuliwa kuwa Jaji Mkuu.

Luhanjo alisema Mallaba kabla ya uteuzi huo, alikuwa Mkurugenzi wa Sehemu ya Mikataba katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #8 2011-12-23 21:28
Hongera Lubuva Kwa Uteuzi huo.
Quote
 
 
0 #7 2011-12-23 16:55
Naye Jaji Lubuva ni kada wa CCM, huyu alipokuwa mwanasheria wa serikali aliwahi kupigia sheria kura. Ndiyo hao hao makada wa CCM. Hawezi kudhibiti wizi wa kura. Amewekwa kulinda maslahi ya CCM. Pole sana wanaharakati tumepata kibaraka mwingine atakayeweka CCM madarakani kwa njia zozote.
Quote
 
 
0 #6 2011-12-23 16:55
Hao tumewazoea, huyo makame amemaliza wapi utumishi wa umma semeni amemaliza kazi aliyopewa na chama siyo taifa maana kwa kipindi chake tuliona madudu mengi tuu kwenye tume ya uchaguzi. Kwa nini asiteue vijana hao wazee amewapendea nini? Ngoja tuone na hawa watatufikisha wapi.
Quote
 
 
0 #5 2011-12-23 15:20
Quoting maganga:
Bw Mallaba ni sehemu kubwa katika kufanikisha mikataba mibovu ya serikali inayofilisi nchi, Leo hii kapewa tume ya uchaguzi hapo sina la kujumlisha wala kutoa.


Mmhh!! Yetu macho kama hii nchi haitaangukia kwenye machafuko 2015. Kwa mtindo huu, Mola atuepushie shari tu. Yajayo, ya mafuriko haya ni rasharasha.
Quote
 
 
0 #4 2011-12-23 14:22
mh anaendelea kurudisha fadhila watu pipooooooo
Quote
 
 
0 #3 2011-12-23 14:14
Mngependa Rais amchague nani kuwa mwenyekiti na Makamu tume ya uchaguzi na nani awe katibu
Quote
 
 
-1 #2 2011-12-23 11:20
MAKAME HAKUWA MTUMISHI WA UMMA ALIKUWA MTUMISHI WA CHAMA AMBAPO AMEKAMILISHA KAZI ALOKUWA AMETUMWA VIZURI HONGERA LUIS MAKAME NA KIRAVU KWA KAZI NZURI......
Quote
 
 
-1 #1 2011-12-23 04:18
Bw Mallaba ni sehemu kubwa katika kufanikisha mikataba mibovu ya serikali inayofilisi nchi, Leo hii kapewa tume ya uchaguzi hapo sina la kujumlisha wala kutoa.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner