MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Siasa CUF wamng’ang’ania Raza
BOOKMARK THIS PAGE
CUF wamng’ang’ania Raza  Send to a friend
Saturday, 28 January 2012 09:06

Talib Ussi, Zanzibar
MGOMBEA wa Chama  Cha Wananchi (CUF) katika uchaguzi mdogo wa kiti cha uwakilishi wa Jimbo la Uzini, mjini Zanzibar, Salma Husein Zarali, amekata rufaa katika Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kupinga uamuzi uliotolewa na ofisi tume hiyo katika  Wilaya ya Kati Unguja, kuhusu mgombea wa CCM, Mohamed Raza.

Mgombea huyo wa CUF alikuwa amewasilisha katika ofisi hiyo, pingamizi la kutaka Raza  aondolewe katika kinyang’anyiro hicho kwa madai kuwa amekosa sifa za kumwezesha kugombea.
 
Salma alitoa msimamo huo jana, alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hii, huko  Uzini.Mgombea huyo wa CUF alisisitiza kuwa Raza amevunja sheria ya  uchaguzi namba 46  kifungu kidogo 3 (a) na kuitaka tume itumie kifungu cha 44 (4) kumwengua.
 
Alidai kuwa mgombea yeyote wa nafasi ya uwakilishi wa jimbo, anapaswa kula kiapo mbele ya hakimu wa mkoa, lakini Raza amekula kiapo chake mbele ya hakimu wa wilaya.
 
“Sisi  tunaenda mbele zaidi kudai haki yetu ya msingi dhidi ya mgombea huyu ambaye kimsingi  hastahiki kugombea kwa kuwa amekiuka sheria,” alisema  Salma.
 
Jana ofisi ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar katika Wilaya ya Kati ilitupilia mbali pingamizi zilizowasilishwa na  CUF na Chadema dhidi ya Raza, kwa maelezo kwamba kisheria madai yao hayana msingi.
 
Lakini Salma alisema kama tume itaendelea kumbeba Raza, wao watakwenda mahakamani kuomba uchaguzi usitishwe hadi hapo sheria zitakapofuatwa.“ Kama wakiendekleza na msimamo wa wao, sisi tutakwenda kudai haki mahakamani,” alisema.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
  • Kupiga Kura

  • Jumapili


Ajali ya Meli ZnZ inatufundisha nini?