|
Tausi All WAHAMIAJIRI haramu wanane kutoka nchi za Pakistan, Bagladeshi na Afrika Kusini, wameamriwa kuondoka nchini ndani ya siku saba.
Amri hiyo ilitolewa jana na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam.Wahamiaji hao ambao kuondoka kwao kutasimamiwa na Idara ya Uhamiaji, wametajwa ni Rizwan Fazal, Barbar Hussain na Riaz Nagash.
Wengine ni Talha Khaid, Imran Hossain, Habibur Rahman, Esrat Molla na Hussain Amjad.Wahamiaji hao walikuwa wamehifadhiwa katika maeneo la Kariakoo kinyume cha sheria.Inadaiwa kuwa kitendo hicho kilifanywa kwa ushirikiano wa Mohamed Fazal na mkewe Fatma Fazal ambao wamehukumiwa kifungo cha miezi mitatu jela au kulipa faini ya Sh100,000 baada ya kupatikana na hatia.
Wakati huo huo, mahakama hiyo pia imewahukumu kifungo cha miaka mitano jela, Issa Mkorea (26) na Abeid Seleman(26) baada ya kupatikana na hatia ya kula njama, kuingilia njia za mawasiliano za TTCL na kuisababishia hasara ya Sh32.5 milioni.
Akisoma hukumu jana, Hakimu Mkazi, Liad Chamshama ,alisema katika shtaka la kula njama washtakiwa watatumikia kifungo cha mwaka mmoja jela.
Alisema katika shtaka la kuingilia njia za mawasiliano za TTCL na kuisababishia hasara ya Sh 32.5 milioni, watatumikia kifungo cha miaka mitano jela na kwamba katika shtaka la kujipatia huduma kwa njia ya udanganyifu, pia watatumikia kifungo cha miaka mitano jela.
Hakimu Chamshama alifafanua kuwa vifungo hivyo vyote vitakwenda sambamba na kwa hiyo watatumikia kifungo cha miaka mitano jela kwa kila mmoja.
Hukumu hiyo ikwisha tolewa na hakimu mstaafu, Ezron Mwankenja Januari 2009 lakini washtakiwa hao na wenzao Maulid Ntandu, Issa , Abeid Seleman, Jumanne Rashid na Salvius Anjelius walikuwa wameruka dhamana na kutoroka. Kwa upande wa Issa na Abeid walitorokea mkoani Singida hadi walipokamatwa na Inspekta Ally Kimweri na Koplo Elias Israel.
|