MwanzoContactsEmail
Home Habari Mahakamani Mkurugenzi halmashauri Moshi kizimbani kwa uhujumu uchumi
BOOKMARK THIS PAGE
Mkurugenzi halmashauri Moshi kizimbani kwa uhujumu uchumi  Send to a friend
Wednesday, 25 January 2012 23:10

Daniel Mjema, Moshi
TAASISI ya kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imewaburuza kortini vigogo wawili wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi Vijijini (MDC), wakikabiliwa na makosa mawili ya uhujumu uchumi.

Vigogo hao waliofikishwa mbele ya Hakimu Mkazi, Mariam Lusewa ni Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Annah Mwahalende na Kaimu Mkuu wa Idara ya Rasilimaliwatu, Sadik Mrisho.

Kwa kawaida kesi za uhujumu uchumi husikilizwa na Mahakama Kuu ya Tanzania, isipokuwa, zinaweza kusikilizwa na mahakama ya hakimu mkazi kama Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) atatoa idhini.

Katika kesi hiyo, tayari DPP alishatoa idhini hiyo Desemba 16, mwaka jana ili tuhuma zinazowakabili vigogo hao ambazo ni kinyume cha kifungu namba 12(3) sura ya 200 ya sheria ya uhujumu uchumi kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2002, isikilizwe na mahakama hiyo.

Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Susan Peter, alidai mahakamani hapo juzi kuwa, makosa yanayowakabili watumishi hao wa umma, waliyatenda kwa pamoja kati ya Desemba 2006 na Machi mwaka jana.

Katika shtaka la kwanza, Susan anayesaidiana na Maghela Ndimbo, alidai kuwa katika kipindi hicho, washtakiwa hao kwa uzembe wa makusudi walishindwa kumchukulia hatua za nidhamu Mhudumu wa Afya wa Zahanati ya Lole aliyetajwa kuwa ni Frank Lyimo.

Waendesha mashtaka hao walidai, licha ya mtumishi huyo kutokuwapo kituo chake cha kazi kuanzia Aprili,2006 hadi Novemba, 2008, washtakiwa hawakumchukulia hatua za nidhamu.

Katika shtaka la pili, ilidaiwa kati ya Desemba, 2008 na Machi, mwaka jana washtakiwa hao walishindwa kutimiza majukumu yao kwa busara na kuisababishia Halmashauri ya Moshi kupata hasara ya Sh2.75 milioni.

Washtakiwa wote walikana mashtaka hayo na kuachiwa kwa dhamana  kwa sharti ya kila mmoja kuwa na mdhamini mmoja ambaye ni mtumishi wa Serikali mwenye kitambulisho.

Washtakiwa hao walitimiza sharti hilo na kesi hiyo iliahirishwa hadi Februari 28, mwaka huu itakapotajwa tena.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #6 2012-01-26 22:46
TAKUKURU kwa kiasi kikubwa ni wanafiki na ni wala rushwa wakubwa sana hapa nchini.Kwa maana ya kwamba wapo vigogo wanaotafuna nchi yetu mpaka imefikia mwisho imekonda kuliko maelezo lakini hawa jamaa hubaki kukimbizana na vitu vidogo tu.Unakimbia kumshitaki mkurugenzi eti alishindwa kumchukulia hatua mfanyakazi wakati wapo watu wanaojilimbikiz ia mali za umma hamuwachukulii hatua yoyote.Mnanikera sana,acheni unafiki na uchawi,fanyeni kazi kistaarabu
Quote
 
 
0 #5 2012-01-26 16:47
Tunaomba TAKUKURU ifanye uchunguzi zaidi hapo halmashauri ya moshi kuna mambo mazito zaidi ya ufisadi na uhujumu uchumi ni pamoja na huduma mbaya kwa wananchi.
Mwanzo mzuri huwa na mwisho mzuri haya ni mashina lazima tuchambue zaidi mti mzima na matawi yake.Tumwogope mung jamii na wananchi wanamatatizo mengi tuwasaidie. Big up TAKUKURU
Quote
 
 
0 #4 2012-01-26 14:22
Ninyi TAKUKURU,Acheni kushughulikia dagaa huku mkiacha 'papa' na 'sangara' wakiendelea kujidai na kuila nchi.
huu ni unafiki na hakika hamfanyi kazi zenu kama inavyotakiwa iwe.
Mission na vision ya taasisi yenu imebaki kwenye makaratasi tu.shem upon you PCCB!
Quote
 
 
0 #3 2012-01-26 14:16
Quoting saleh:
Hizi kesi za kinafiki ndizo zinazozidi kutukerehesha wananchi. Hawa ndiyo wanaoidaiwa wanahujumu uchumi? Wale akina Mramba na Yona walioisababishi a serikali kukosa mabilioni ya fedha na pia kununua rada kwa bei za uongo, wanashitakiwa kwa kesi ya madaraka. Hii nchi lazima kitaeleweka siku moja.

Jesus come soon! Tufunge macho na masikio.............Hali ni mbaya kuliko tunavyoona na tunavyosikia. Kila mahali ni drama tupu. Nakubaliana nawe.....ipo siku moja kitafahamika tu!
Quote
 
 
0 #2 2012-01-26 13:17
Saleh uko sawa kabisa, one day yes!!!
Quote
 
 
+3 #1 2012-01-26 11:08
Hizi kesi za kinafiki ndizo zinazozidi kutukerehesha wananchi. Hawa ndiyo wanaoidaiwa wanahujumu uchumi? Wale akina Mramba na Yona walioisababishi a serikali kukosa mabilioni ya fedha na pia kununua rada kwa bei za uongo, wanashitakiwa kwa kesi ya madaraka. Hii nchi lazima kitaeleweka siku moja.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner