MwanzoContactsEmail
Home Habari Mahakamani Wabunge wazoa Sh90mil kila mmoja
BOOKMARK THIS PAGE
Wabunge wazoa Sh90mil kila mmoja  Send to a friend
Tuesday, 15 February 2011 07:35

Mwandishi Wetu, Dodoma

JUMLA ya Sh3.24 bilioni zimelipwa kwa wabunge ili kuwawezesha kununua magari binafsi kwa ajili ya shughuli za kibunge, imeelezwa.

Kwa mujibu wa habari hizo kila mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amelipwa Sh90 kwa ajili ya kujinunulia gari.

Aidha, wabunge hao wapatao 360 wamekatiwa bima ya afya inayotarajiwa kuanza kutumika kabla ya mwezi Juni mwaka huu.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika uzinduzi wa Tawi la Chadema, Mipango Kata ya Miyuji mkoani Dodoma wabunge wa Chadema, walisema kuwa wanashangazwa na hatua ya Rais Kikwete kuweka pikipiki za matairi matatu (Bajaji) kama moja ya vipaumbele vyake ili zitumike kubeba wajawazito wakati wabunge wanalipwa mamilioni.

Katika hotuba yake ya kulizindua bunge Kikwete alieleza mpango wa serikali yake kununua pikipiki hizo 400 zitakazosambazwa maeneo mbalimbali hasa vijijini kwa ajili ya kuwabebea wajawazito kama njia ya kupunguza matatizo ya usafiri kwenye maeneo hayo.

"Ndugu zangu hali ni mbaya, siku moja tutafanya maandamano bungeni, sio kutoka nje ya ukumbi. Inashangaza, tumepewa Sh90 milioni za magari kwa wabunge wote, huku bungeni tunajadili bajaji kuwa 'ambulance'(gari ya kubebea wagonjwa),'" alisema mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema.

Alisema mbali na hilo katika hali inayoonyesha kuwa hospitali za serikali ni mbaya, katika semina iliyofanyika Dar es Salaam hivi karibuni, wabunge waliomba kuwekewa bima za afya, kutibiwa nje ya nchi na katika hospitali binafsi hapa nchini.

"..Wabunge tumeomba 'insurance' (Bima) kila mmoja amepewa na kabla ya Juni naamini zitaanza kutumika, tumeomba kutibiwa 'private hospital' (hospitali binafsi). Hii inaonyesha hospitali za serikali zilivyo mbaya na hao wenye uwezo wanazikimbia," alisema Lema.

Aliongeza kuwa: Ndoto ya kuiondoa CCM ni 'serious' (thabiti), lakini mkifanya noma ya kupata haki, hiyo imebarikiwa. Kama (CCM) wanafikiri wanaweza kuendesha nchi watakavyo, sasa hawawezi, ninyi vijana msipojitoa kwa sasa nchi itakufa."
 
Alikwenda mbali zaidi akisema anaomba wake za viongozi wapate ujauzito na kupakiwa katika bajaji hizo wakati wa uchungu kwenda kujifungua ili waone adha ya usafiri huo itakavyokuwa.

Akiongea katika mkutano huo naye mbunge Tundu Lissu aliwataka wananchi kutoogopa mabadiliko na kwamba historia haiheshimu watu wanaoogopa.

""Historia haiheshimu wanaoogopa, tusije kusahau bei ya mabadiliko, bei yake ni kupigwa, kufungwa hata bei kubwa zaidi ya kifo," alisema Lissu.

Naye John Mnyika alisema Chama chake kitaandaa kongamano maalumu la vijana wa vyuo vikuu ili wapate muda wa kuzungumza nao vizuri na kwamba maandamano ya kuishia viwanjani yametosha na sasa watakuwa wakifika kwa wahusika.

"..Maandamano ya kuishia viwanjani imetosha, sasa tutaenda maeneo ya wahusika, vyuo lazima mjenge mtandao
imara, lazima mpambane na umasikini," alisema Mnyika.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
+1 #21 2011-02-16 01:41
Mimi nionavyo ni kwamba bunge limekuwa mtambo wa kufilisi nchi. 90 milioni x wabunge 300 = 27000,000,000.00/= za magari tu. Pesa hii ina uwezo wa kujenga shule za sekondari 76 au zahanati 100. Halafu mishahara MNONO bila kusahau posho za vikao wakati watu wengi hasa vijana hawana ajira?, matibabu katika hospitali binafsi na walalahoi wananunuliwa bajaji? Haya yote yanaonesha kwamba huu mtambo uitwao bunge una matatizo makubwa. Ulafi wa hali ya juu. Ila wakati wao umekaribia maana kizazi cha leo hakitambui babake mtu au fulani katika issue za msingi za kitaifa.
Quote
 
 
0 #20 2011-02-16 01:41
JAMANI! SIELEWI NA SIAMINI KAMA KWELI TZ NCHI YA AMANI, Quote:
DEMOKRASIA
NA MAENDELEOA.
Quote
 
 
+1 #19 2011-02-15 19:56
Wabunge wa Chadema, chukueni hizo milioni 90,nunueni gari kwa milioni 50, milioni 40 saidieni miradi ya majimbo yenu ili watu walio wachagua na wao wafaidike na hayo mamilioni.
Quote
 
 
+1 #18 2011-02-15 19:53
Nyie wabunge wa Chadema ni wanafiki tu, kama kweli muna mapenzi na nchi hii na raia wake, basi hizo hela zote za wabunge wa Chadema zikusanyeni na mukanunue hayo ma-ambulance muyapeleke vijijini. Hapo kweli mutaonyesha kuwa nyinyi ni wazalendo wa kweli na sio longo longo tu.
Quote
 
 
+1 #17 2011-02-15 16:38
tukikokotoa angalau wabunge 300:
300 X Tshs.90,000,000/= ni TshsBilioni 27
Quote
 
 
+2 #16 2011-02-15 15:35
Jaman,wasiwasi wangu ni hao wapinzani kama wanauma na kupuuuliza vile,itaniwea vigumu daima kumuamini mtu yeyote si upinzani na se serikali,hivi nyinyi chadema,kama maneno yenzu yangeambatana na matendo mngeshachukua nchi lakin sera mnazo ambazo zna mlengo wa kuwapatia ulaji pia kama hao wana ccm wenyewe...mfano hizo pesa kama mnezikataaa halafu mkahamasisha maandamano nchi nzima kupinga kitendo hicho cha unyongaji wa wanyonge,jnina uhakika kwa namna ambavyo hata bibi yangu huko sitimbi anavyo wafahamu kwa sasa angewaunga mkono,mnaongea tayari pesa ziko mfukoni hatuwezi kuwaelewa kamwe,hapo unanikumbusha n.cameroon mmoja aliyewahi kuniambia kuwa kila mtu ni mfisadi isipokuwa kama hajapata nafasi ya kufanya hivyo tu,si taki kuwatwika dhambi watu wote ,la hasha naamin kuwa kuna watu wasafi lakin WAPINZANI hamna la kudanganya...niko ughaibuni lakin kila nikitaja kuwa natoka Tanzania nazomewa..ni aibu kubwa,umaskini huku mtu anagawiwa milion 90....Mungu anisamehe lakin kama ningekuwa na uwezo ningefutilia mbali mfumo mzima wa utawala nikajaribu wale ambao hawajaonja hata ubunge...Tanzania inaelekea kubaya...ukimkamua ng'ombe maziwa yakaisha hadi ukataka kukamua na damu akistukia atakupiga teke la kifo,Ihave a dream....''.tanzania muda si mrefu kutachafuka''Take care nyinyi wala mabilioni.....
Quote
 
 
+2 #15 2011-02-15 14:49
Kila chenye mwanzo lazima kiwe na mwisho ipo siku mwisho wao wakutuburuza watakavyo utafika tu, Mungu hawezi kuwa upande wao siku zote.
Quote
 
 
-6 #14 2011-02-15 14:35
hakuna mtu mwenye uchungu na wananchi kama nyinyi wabunge wa upinzani mngekataa hizo pes tungewafikiria ,nyiniy ni wanafiki ambao mmekaa kutudanganya kwa kutupa shilingi 1000/= na kupoteza maisha yetu.Msipokee hizo pesa ama pelekeeni mkajenge hospital ama mnunue magari ya wagonjwa WANAFIKI NYINYI MSHINDWE KABISA [NENO BAYA]
Quote
 
 
-3 #13 2011-02-15 14:24
Sasa kama millioni 90 mnaona siyo za haki mbona mmezichukua? Nyinyi wapinzani msitake kutuletea danganya toto. Hela mnazitaka halafu kujidai unafiki mbele ya wananchi. Zirudisheni basi serikalini ili tuwaelewe.
Quote
 
 
+3 #12 2011-02-15 14:03
Kwakweli tunakoelekea nikubaya. Kama serikali iko tayari kumpatia kila mbunge gari alafu inanunua vibajaji kwa ajili ya mama zetu wajawazito, hii inatisha.
Wito wangu ni kwa vyama vya upinzani kupeleka magari hayo yakatumike kwenye majimbo yoa, nadhani serikali itaona aibu.
Kwakweli kwa style hii, lazima 2015 nitangaze nia.
Quote
 
 
+1 #11 2011-02-15 13:55
nauliza tu,
jamani hivi pesa hizo ,tungeongea na serikali ya japan au germany au kokote mtu afikiriapo, tukawaomba kununua magari ya wabunge kweli ingeshindikana, na pesa zingetumika nyingi namna hiyo?hivi jamani tusioneane aibu, ni nchi gani inayotoa magari ya bei kubwa namna hiyo? nijuavyo mm nchi kadhaa,ukikutan a na wawakilishi wao bungeni unaweza kuona huruma,kama ni daladala wote daladala.sio kusema wasiwe na magari yao, hapana, ila yasiwe ya bei kubwa sana jamani,ina maana baada ya miaka 5 tena wanapewa nyingine!!? kudadeki..eti nchi masikini?
kuna watu hawajui hata umeme ni nini ?
watu hawajui hata maji ya bombani ni nini?
watu hawajui hata hospitali zipo wapi zaidi ya dispensari tu.embu fikirieni upya nyang'au nyie...!
Quote
 
 
+1 #10 2011-02-15 13:51
kwa mwendo huu siasa peke yake ndo inafaa,hakuna cha wakulima,walimu ,watabibu,wanas heria,huko kote njaa,shibe iko bunge,mi naona kusiwe na mgao wa kazi,kazi muhimu ni siasa peke yake.
Quote
 
 
+1 #9 2011-02-15 13:40
Acheni kuiga hakuna mwenye uchungu na nchi,historia inajirudia inaonyesha jinsi gani watu wa asili ya kibantu tusivyo na mismamo,ndo maana utumwa ukatulemea sisi,na si wamisri,sisi wote waoga,uonevu uliotokea nchi ya Tunisia na kusababisha mabadiliko makubwa mpaka misri,unafanyik a kila siku Tanzania,katika nyanja mbalimbali za kimaisha,hatuja liani huo ndio ukweli.
Quote
 
 
+1 #8 2011-02-15 13:35
Pokeeni huo mshiko lakini "the time will tell"
Quote
 
 
+1 #7 2011-02-15 12:54
Tundu Lisu, nakupongeza sana. Una ongea ukweli tene kwa uchungu amabao naamini utaleta mabadiliko makubwa nchini Tanzania. Mungu akuongezee busara na uchungu kuhusu nchi yetu ili utimize shughuli zako za kuwakilisha wananchi kwa umakini mkuu. Pia fahamu kwamba, wapo wananchi kama wewe (mimi nikiwa mmojawapo) wanaojua gharama za kutafuta haki.

Mungu atainua majemedari watakaosimama nawe pamoja na wengine kama Dr Slaa, Mbowe, Mnyika, Mdee na wengine wanaosononeka juu ya umasikini unaoendelezwa na watawala walioko madarakani. Pamoja tutasimama na kushinda. Ngoma ya utawala sasa inalia sana maana kupasuka kwake kumekaribia. Mungu ibariki Tanzania.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner