ACT wamjibu Ole-Sendeka

Dar es Salaam. Chama cha ACT-Wazalendo kimefungua milango kukaribisha uchunguzi juu ya mali na madeni ya kiongozi wake mkuu Zitto Kabwe.
Akizungumza na waandishi wa habari Katibu wa Kamati ya Bunge na Serikali za Mitaa ya ACT, Habib Mchange alisema chama hicho hakina shaka kwamba kiongozi wake ni msafi.
"Tunavitaka vyombo vya uchunguzi vianze kazi hiyo mara moja na tutafurahi ukihusisha pia akaunti zake binafsi "alisema Mchange