ANC yathibitisha inamjadili Zuma

Muktasari:

"Hakuna muda uliowekwa...Hatufanyi kazi kwa mtindo huo, tunashikiana, tunajadili,” aliongeza Magashule kwamba hakuna uamuzi wa mwisho uliowekwa kuhusu kuondoka kwa Zuma.

Johannesburg, Afrika Kusini. Chama tawala cha African National Congress kimethibitisha kwamba mazungumzo yanaendelea kuona namna Rais Jacob Zuma atakavyoondoka ofisini bila shaka ikiashiria mwanzo wa mwisho wa kashfa zilizodumu miaka tisa ya utawala wake.

Zuma amekuwa akikabiliwa na shinikizo la kumtaka ajiuzulu tangu alipoachia uaongozi wa ANC kwa makamu wake Cyril Ramaphosa.

 Kashfa

Halmashauri kuu “ilijadili suala hili...kutakuwa na majadiliano kati ya maofisa, Rais Zuma na kwa chama Ramaphosa," alisema Katibu Mkuu Ace Magashule.

"Hakuna muda uliowekwa...Hatufanyi kazi kwa mtindo huo, tunashikiana, tunajadili,” aliongeza Magashule kwamba hakuna uamuzi wa mwisho uliowekwa kuhusu kuondoka kwa Zuma.

Urais wa Zuma ulikumbwa na kashfa za rushwa na ulichafuliwa na kudorora kwa uchumi hali iliyochangia chama kukosa kuungwa mkono kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2019.

Wafuasi wa Ramaphosa wanafanya kampeni atawazwe sasa kama rais na ajaribu kufufua uchumi kabla ya uchaguzi mkuu ambao ANC inaweza kupoteza udhibiti wake kwa mara ya kwanza tangu ulipokomeshwa utawala wa ubaguzi wa rangi.