ATCL kupata ndege mpya Septemba

Muktasari:

"Kama ilivyo dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano tutahakikisha hatua za ununuzi wa ndege mpya zinafanyika kwa haraka ili kuweza kulifufua shirika letu la ndege na kuweza kuanza kutoa huduma za usafiri wa anga ifikapo mwezi Septemba mwaka huu," amesema

Dar es Salaam. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,  Profesa Makame Mbarawa amesema Serikali imelipa Sh36 bilioni, sawa na asilimia 40 kwa ajili ya kununua ndege mbili za shirika la ndege la ATCL.

"Kama ilivyo dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano tutahakikisha hatua za ununuzi wa ndege mpya zinafanyika kwa haraka ili kuweza kulifufua shirika letu la ndege na kuweza kuanza kutoa huduma za usafiri wa anga ifikapo mwezi Septemba mwaka huu," amesema

Waziri huyo ametoa kauli hiyo alipokuwa akikagua ujenzi wa uwanja wa ndege wa Dodoma na kusema kuwa ameridhishwa na maendeleo ya upanuzi wake.

 "Mradi huu umetupa mfano kama tukijipanga vizuri hata kwenye miradi mingine tunaweza kutekeleza kwa haraka na ubora unaotakiwa, kwa upande wetu kama Serikali tutahakikisha uwanja huu unakamilika haraka ili kuruhusu ndege kubwa kuanza kutua," amesema.

Kwa taarifa zaidi nunua gazeti lako la Mwananchi au soma mtandaoni kupitia www.epaper.mcl.co.tz