Ahadi ya umeme kila kijiji yatajwa kuwaharibia wabunge kwenye uchaguzi
Muktasari:
Dodoma. Mbunge wa Bukoba Mjini (Chadema), Wilfred Lwakatare amesema kauli ya Serikali ya kupeleka umeme kila kijiji ni ya uongo, itawaweka katika wakati mgumu wabunge kwenye chaguzi mbalimbali nchini.
Akizungumza jana Mei 24, 3018 katika mjadala wa bajeti ya Wizara ya Nishati mwaka 2018/19, Lwakatare amesema kauli hiyo haifanani na kasi ya usambazaji wa umeme vijijini kwa maelezo kuwa miradi mingi inapangwa kwa ajili ya chaguzi mbalimbali, kusababisha kutotekelezwa.
“Miradi mingi inapangwa kwa ajili ya uchaguzi. Haiwezi kutekelezekwa, ukimsikiliza waziri (Dk Medard Kalemani-Waziri wa Nishati) anavyozungumza kuwa kila kijiji kitapelekewa umeme si kweli. Hoja hii haitekelezeki na itatuweka pabaya tutakapoulizwa (na wananchi),” amesema.
“Ni vyema Serikali ikawaambia wananchi kuwa watachukua umeme mahali utakapopitishwa kuliko kusema watapeleka umeme kila kijiji. Kupeleka umeme kila kijiji hakutekelezeki ni uongo uliokubuhu.”