Azam wataka mechi za Simba, Yanga Chamazi
Muktasari:
Ofisa Habari wa Azam, Jafar Idd amesema wameandika barua kwa TFF wakitaka michezo yao ya nyumbani dhidi ya timu hizo ifanyike Chamazi na si Uwanja wa Taifa kama ilivyozoeleka.
Dar es Salaam. Uongozi wa Azam umeliandikia barua Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuomba michezo yake ya nyumbani ya Ligi Kuu dhidi ya Simba na Yanga ifanyike kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Ofisa Habari wa Azam, Jafar Idd amesema wameandika barua kwa TFF wakitaka michezo yao ya nyumbani dhidi ya timu hizo ifanyike Chamazi na si Uwanja wa Taifa kama ilivyozoeleka.
“Uwanja wa wetu umekidhi vigezo vyote vinavyostahili kwa mujibu wa kanuni na taratibu za Shirikisho la Soka Afrika (CAF),” amesema Idd.
Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas hakuwa tayari kuthibitisha taarifa hizo.