Bilionea 'Mo' Dewji apatikana

Mohammed Dewji ‘Mo’

Muktasari:

Mohamed Dewji 'Mo' amepatikana alafajiri ya leo Jumamosi Oktoba 20,2018.

Dar es Salaam. Mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania, Mohammed Dewji ‘Mo’ amepatikana akiwa hai.

Akizungumza na Mwananchi alfajiri ya leo Oktoba 20, 2018, Baba mzazi wa Mo Dewji, Gullam Dewji amesema,"Ni kweli Mo amepatikana, yupo hapa nyumbani."

Mo amepatikana ikiwa ni siku ya tisa tangu alipotekwa na watu wasiojulikana alfajiri ya Oktoba 11,2018 katika Hoteli ya Collosium jijini Dar es Salaam alikokuwa amekwenda kufanya mazoezi.