Boti yazama, sita wafariki dunia

Muktasari:

  • Polisi nchini humo wamethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa juhudi za kuwatafuta abiria wengine waliokuwa kwenye boti hiyo zinaendelea.

Watu sita wamefariki dunia na wengine 16 hawajulikani walipo baada ya boti ya abiria kuzama jana, Jumapili katika mji wa Kaskazini Magharibi mwa nchini ya Colombia.

Polisi nchini humo wamethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa juhudi za kuwatafuta abiria wengine waliokuwa kwenye boti hiyo zinaendelea.

Kwenye uokoaji huo boti ndogo, helikopta zilitumika kuhakikisha majeruhi wanaokolewa haraka. Zaidi ya watu 20 wamekimbizwa hospitalini katika mji wa Guatapé.

Imeelezwa kuwa boti hiyo iliyozama muda mfupi baada ya kung’oa nanga ilikuwa imebeba abiria 150.

Hata hivyo, kiongozi wa idara ya zimamoto waliokuwa wanafanya harakati za uokoaji, Luis Morales amesema chanzo cha ajali hiyo bado hakifahamika.

"Hatujafahamu kama kiini cha ajali hiyo ni tatizo ya kimitambo, ubeba watu kupita kiasi au mawimbi ziwani,"amesema.

Chanzo BBC.