Bulaya atinga tena kituo kikuu cha polisi

Muktasari:

Bulaya amefika polisi saa 1:30 asubuhi

. Mbunge wa Bunda Mjini (Chadema), Ester Bulaya ameripoti kituo kikuu cha polisi cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam leo Aprili 16, 2018 saa 1:30 asubuhi akiitikia wito wa polisi.

Bulaya amesema bado hajaelezwa chochote.

"Ninaendelea kusubiri nipate maelekezo kujua kinachoendelea,” amesema.