CCM yapita bila kupingwa Korogwe Vijijini

Muktasari:

  • Jimbo la Korogwe Vijijini limekuwa wazi kutokana na kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Stephen Ngonyani au Majimarefu

Mgombea wa ubunge Korogwe Vijijini (CCM), Timotheo Mzava amepita bila kupingwa.

Mzava amepita bila kupingwa baada ya muda wa mwisho wa kurejesha fomu leo Agosti 20, 2018 kuwa peke yake.

Akizungumza leo jioni, msimamizi wa uchaguzi katika jimbo hilo ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Korogwe, Dk George Nyaronga amesema, “mgombea wa CCM amepita bila kupingwa.”

Jimbo la Korogwe Vijijini limekuwa wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Stephen Ngonyani maarufu kama Maji Marefu.