VIDEO: Costech yasikitika barua waliyowaandikia Twaweza kusambaa mitandaoni
Muktasari:
Wamebaini barua hiyo waliyowaandikia Twaweza ni ya kwao.
Dar es Salaam. Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) imesikitishwa na kitendo cha barua yake kwenda Taasisi ya Utafiti ya Twaweza kusambaa mitandaoni.
Costech imesema hayo leo Julai 12, 2018 katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo, Dk Amos Nungu amesema baada ya kufuatilia, wamebaini barua hiyo waliyowaandikia Twaweza ni ya kwao.
"Tunasikitika kuona mawasiliano halali ya kiofisi yanapelekwa mitandaoni, hata kabla ya kujibiwa rasmi," amesema Dk Nungu
Kaimu Mkurugenzi huyo amesema barua hiyo si ya kwanza na wamekuwa wakiandika kwenda kwa wadau mara kadhaa.
Naye Mwanasheria wa Costech, Zainab Bakari ameshindwa kufafanua vifungu vya sheria walivyotumia akisema:
"Hatujaja hapa kuzungumzia barua ya Twaweza."
Soma Zaidi: