Diamond kutumbuiza kwenye mashindano ya AFCON
Muktasari:
Diamond ni miongoni mwa wasanii teule watakaotumbuiza katika hafla hiyo.
Dar es Salaam. Wizara ya Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo na Kampuni ya DSTV zimefanikisha safari ya mwanamuziki wa kizazi kipya Diamond Platnumz ya onyesho lake katika ufunguzi wa mashindano ya AFCON nchini Gabon.
Diamond ni miongoni mwa wasanii teule watakaotumbuiza katika hafla hiyo.
Akizungumza wakati akimkabidhi bendera ya Tanzania, Waziri wa Wasanii, Nape Nnauye amesema Tanzania imepata nafasi ya pekee kupata mshiriki kupitia sanaa ya muziki.
"Hii inaonyesha namna sanaa yetu inavyozidi kukua siku hata siku, Diamond amekuwa miongoni mwa wasanii watatu Afrika watakaotumbuiza live wimbo maalum katika mashindano haya, ambao pia utatumika katika mashindano hayo," amesema Nape.