Diwani mwingine Chadema ajiuzulu

Muktasari:

Amesema amechukua uamuzi huo wa hiyari

 


Moshi. Wimbi la madiwani wa Chadema kujiuzulu linazidi kushika kasi na leo Jumanne Agosti 21, 2018 amejiuzulu diwani wa chama hicho kata ya Korongoni manispaa ya Moshi, Ally Mwamba.

Kwa mujibu wa barua ya Mwamba aliyoiandika leo kwenda kwa mkurugenzi wa manispaa ya Moshi, anaeleza kuwa ameamua kujiuzulu bila kushurutishwa na mtu yeyote, kusisitiza kuwa hana zaidi ya hapo, kusisitiza kuwa amechukua uamuzi huo wa hiyari.

Katibu wa Chadema Mkoa wa Kilimanjaro, Bazil  Lema amesema chama hicho kikuu cha upinzani nchini kimepokea barua ya diwani huyo.