Dk Mashinji asema haumwi

Muktasari:

Dk Mashinji akizungumza na Mwananchi muda mfupi baada ya kuwa kuripotiwa kuwa ameugua ghafla na kupelekwa  Hospitali ya Amana.

Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji amesema yeye ni mzima na huenda kuna makosa yametokea kumuhusisha yeye kuwa ni mgonjwa.

Dk Mashinji akizungumza na Mwananchi muda mfupi baada ya kuwa kuripotiwa kuwa ameugua ghafla na kupelekwa  Hospitali ya Amana.

Amesema kuwa yeye ni mzima na anakula ugali. Hivi sasa yuko katika kikao cha Kamati Kuu ya Chadema inayoendelea jijini Dar es Salaam.