Gwajima ajipanga kununua treni ya umeme

Muktasari:

Gwajima ameyasema hayo leo katika ibada ya Jumapili  huku akimsifu Rais Magufuli kwa kuchukua hatua hiyo.

Dar es Salaam. Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amesema amedhamiria kununu treni ya umeme  baada ya Rais John Magufuli kuonyesha dhamira ya kujenga reli  ya kisasa(standard gauge).

Gwajima ameyasema hayo leo katika ibada ya Jumapili  huku akimsifu Rais Magufuli kwa kuchukua hatua hiyo.

Alisema licha yeye ni mchungaji wa Taifa na anaamini ipo siku Dar es Salaam yote itakwenda kanisani kwake kusali.