Hollande amshambulia Trump kwa maneno

Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani, Donald Trump

Muktasari:

Hollande amemshutumu Trump kutokana na matamshi yake makali dhidi ya wazazi wa mwanajeshi wa Marekani aliyefia vitani nchini Iraq akisema yanatia fedheha.

PARIS. Rais wa Ufaransa, Francois Hollande amemshambulia hadharani mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani, Donald Trump akiyataja matamshi yanayotolewa na mgombea huyo kama yanayotia kichefuchefu.

Hollande amemshutumu Trump kutokana na matamshi yake makali dhidi ya wazazi wa mwanajeshi wa Marekani aliyefia vitani nchini Iraq akisema yanatia fedheha.

Rais wa Marekani, Barack Obama pia amemtaja Trump kuwa mtu asiyestahili kuwa Rais wa Marekani na kuwahimiza vigogo wa Republican kutomuunga mkono mgombea huyo kwani hana uelewa wa masuala ya kiuchumi na ya kigeni.