JPM amteua Dk Mduma mwenyekiti wa CMSA
Muktasari:
Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dk Mduma umeanza Februari 23, mwaka huu.
Dar es Salaam. Rais John Magufuli leo (Ijumaa) amemteua Dk John Mduma kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).
Taarifa iliyotolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dk Mduma umeanza Februari 23, mwaka huu.
Dk Mduma anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Grace Rubambey ambaye amemaliza muda wake.