JPM awasili viwanja vya Jamhuri kwa sherehe za Muungano
Muktasari:
Viongozi wengine, wakiwamo mawaziri na wabunge walifika katika uwanja huo kuanzia saa 1:20 hadi saa 1:30 asubuhi.
Dodoma. Rais John Magufuli amewasili katika viwanja vya Jamhuri kwa ajili maadhimisho ya sherehe za miaka 53 ya Muungano.
Rais amewasili saa 3; 15 akiwa kwenye gari la wazi.
Viongozi wengine, wakiwamo mawaziri na wabunge walifika katika uwanja huo kuanzia saa 1:20 hadi saa 1:30 asubuhi.
Kiongozi wa kwanza kuwasili ni Waziri Kiongozi Mstaafu Shamsi Vuai Nahodha ambaye alifika saa 1:25 asubuhi akifuatiwa na Waziri Mkuu Mstaafu John Malecela aliyefika saa 1:30 asubuhi.
Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete aliwasili saa 2:20 asubuhi.
Uwanja wa Jamuhuri umepambwa kwa rangi za bendera ya Taifa na watu wote wanaoingia wamegawiwa bendera za Taifa ndogo za mkononi.
Watu walianza kuingia uwanjani saa 12: 30 asubuhi kwa kutumia mageti kadhaa ambayo yalipangwa kutumika kwa ajili ya kupita wageni.