Kauli ya Kikwete UDSM yazua mjadala mitandaoni

Rais mstaafu wa awamu ya nne ambaye pia ni kuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jakaya Kikwete akiteta jambo na Makamu Mkuu wa Chuo cha Dar es Salaam, Prof Rwekeza Mukandala.

Muktasari:

Kikwete alisema maneno hayo kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakati akizungumzia mambo anayokusudia kuyafanya akiwa mkuu mpya wa taasisi hiyo.

Dar es Salaam. Mitandao ya kijamii jana ilisheheni sehemu ndogo ya hotuba ya Rais mstaafu, Jakaya Kikwete ikieleza mambo ambayo kiongozi mpya anatakiwa kuyafanya.

Kikwete alisema maneno hayo kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakati akizungumzia mambo anayokusudia kuyafanya akiwa mkuu mpya wa taasisi hiyo.

“Unapokuwa mpya ni lazima watu waone kuna mambo mapya. Lakini mapya ya maendeleo,” alisema na kutulia akiangalia hadhira na baadaye kutabasamu.

“Na sio mapya ya kubomoa kule tulikotoka,” alisema na kutoa kicheko kabla ya kuendelea kusoma hotuba yake iliyoandikwa kwa lugha ya Kiingereza.