Hisa na Paundi zadoda Uingereza

Muktasari:

Mara baada ya tukio hilo la kihistoria, kiwango cha hisa cha makampuni makubwa 100 yaliyojiorodhesha katika soko la hisa la London kimeporomoka kwa zaidi ya asilimia nane kabla ya kupanda hadi pungufu ya asilimia nne.

Soko la hisa la London limeanguka ghafla ikiwa ni saa chache kupita baada ya matokeo ya Uingereza kujiondoa Jumuiya ya Ulaya (EU) kupitia sanduku la kura kutangazwa mapema leo.

Mara baada ya tukio hilo la kihistoria, kiwango cha hisa cha makampuni makubwa 100 yaliyojiorodhesha katika soko la hisa la London kimeporomoka kwa zaidi ya asilimia nane kabla ya kupanda hadi pungufu ya asilimia nne.

Katika sekta ya fedha, kibenki za Barclays na RBS hisa zimeshuka kwa karibu asilimia 30 lakini hali imerudi na kuwa asilimia 20.

Mapema leo, Paundi ya Uingereza iliporomoka kwa kasi mara baada ya matokeo hayo yalipotangazwa. Anguko hilo ni mara 10 tangu sarafu hiyo ishuke kwa kasi 1983.

Hata hivyo, baadaye leo mchana sarafu hiyo ilipanda lakini ikiwa iko chini bado kwa asilimia nane.

 “Suala la Uingereza kujitoa EU limeleta wingu katika uchumi wa dunia kwa takribani mwezi mmoja sasa na sasa wingi limekuwa giza kabisa,” amesema Denis de Jong, mkurugenzi wa UFX.com.

BBC