Marekani yatuma jeshi Iraq

Muktasari:

Nyongeza hiyo itafanya idadi ya wanajeshi wa Marekani walioko nchini Iraq kufikia 4650.

Uamuzi huo ulitangazwa na Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Ashton Carter akiwa nchini Iraq kwa ziara ya ghafla baada ya kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Haider al-Abadi.

Baghadad, Iraq. Marekani imeamua kutuma wanajeshi wengine 560 nchini Iraq kusaidia kupambana na kundi la Dola ya Kiislamu(IS).

 Nyongeza hiyo itafanya idadi ya wanajeshi wa Marekani walioko nchini Iraq kufikia 4650.

Uamuzi huo ulitangazwa na Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Ashton Carter akiwa nchini Iraq kwa ziara ya ghafla baada ya kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Haider al-Abadi.

Wanajeshi hao 560 ni pamoja na wapiganaji, wahandisi na wafanyakazi wa kawaida .

Wanajesh hao watakuwa karibu na kambi ya jeshi la anga ya Qayyarah. IS imeweka ngome yake nchini Iraq.