Museveni aweka foleni Kampala

Muktasari:

Museveni alikuwa safarini kurejea Kampala akitokea Wilaya ya Isingiro alikokwenda kushiriki maadhimisho ya Siku ya Idadi ya Watu Duniani ambayo hufanyika kila mwaka Julai 11.

Kampala, Uganda. Rais Yoweri Museveni wa Uganda amevuta  hisia za wapita njia pale alipolazimika kusimamisha kwa muda msafara wake ili apate fursa ya kuzungumza na simu.

Museveni alikuwa safarini kurejea Kampala akitokea Wilaya ya Isingiro alikokwenda kushiriki maadhimisho ya Siku ya Idadi ya Watu Duniani ambayo hufanyika kila mwaka Julai 11.

Akiwa njiani kurejea Ikulu, Rais Museveni ghafla aliamuru msafara wake usimame ili azungumze na simu aliyodaiwa kuwa ilikuwa muhimu.

“Tulikuwa katika barabara ya Kyeirumbi kurejea Kampala, ghafla rais aliamuru msafara wake usimame mara moja ili azungumze na simu yake ambayo tulielezwa ilikuwa muhimu,” kilieleza chanzo kimoja cha habari.

Baada ya kusimamisha msafara wake, Rais Museveni alisogea mbele kidogo kisha kuketi katika kitu na kuendelea na mazungumzo yake.

Wakati wote walinzi walikuwa wamesimama kando ya magari yaliyokuwamo kwenye msafara huo huku wengine wakiwa wamesalia ndani ya magari hayo.

Haikuweza kufahamika mara moja kiongozi huyo alikuwa akizungumza na nani wale jambo alilokuwa akilijadili. Barabara ya Kyeirumba yenye umbali wa kilometa 75 inaunganisha Uganda na Tanzania.