Zuma ahusishwa na jaribio la kumuua mkuu wa polisi

Muktasari:

  • Tuhuma hizo zilitolewa bungeni Jumanne na Mbunge wa DA Dianne Kohler Barnard aliyedai maveterani hao walipewa makataba huo baada ya kukutana na rais wa zamani Jacob Zuma, katibu wa chama cha ANC wa KwaZulu-Natal, Super Zuma na aliyekuwa mratibu wa mpito wa ANC ya KwaZulu-Natal, Sihle Zikalala.
  • Akizungumza katika mjadala wa makadirio ya matumizi ya Jeshi la Polisi Kohler Barnard alisema: "Wenzangu, ikiwa mnadhani kwa hatimaye kuondolewa ndani ya Jeshi la Polisi (SAPS) kwa bosi mhuni wa makosa ya jinai Richard Mdluli kimiujiza kulikuwa kumefanikisha kumweka kando ya muunganiko wa serikali kugubikwa na ufisadi, mtakuwa mmekosea.
  • "Kuna uthibitisho kutoka vyanzo vitatu vya kujitegemea na vya kuaminika kuwa mavaterani wa MK kutoka Cornubia karibu na Phoenix huko KwaZulu-Natal walichukuliwa kwa ajili ya kufanya kazi hiyo baada ya mikutano na watu si wengine zaidi isipokuwa rais wa zamani aliyeng’atuliwa Jacob Zuma, Super Zuma na Sihle Zikalala. Dudu Myeni pia amehusishwa baada ya kukutana na maveterani hao," alisema Kohler Barnard

Durban, Afrika Kusini. Tuhuma nzito zimetolewa kwamba maveterani wa zamani wa jeshi la ukombozi ‘Umkhonto weSizwe’ walipewa mkataba wa kumuua mkuu wa zamani wa polisi wa upelelezi wa Jimbo la KwaZulu-Natal Johan Booysen.
Tuhuma hizo zilitolewa bungeni Jumanne na Mbunge wa DA Dianne Kohler Barnard aliyedai maveterani hao walipewa makataba huo baada ya kukutana na rais wa zamani Jacob Zuma, katibu wa chama cha ANC wa KwaZulu-Natal, Super Zuma na aliyekuwa mratibu wa mpito wa ANC ya KwaZulu-Natal, Sihle Zikalala.
Akizungumza katika mjadala wa makadirio ya matumizi ya Jeshi la Polisi Kohler Barnard alidai: "Wenzangu, ikiwa mnadhani kwa hatimaye kuondolewa ndani ya Jeshi la Polisi (SAPS) bosi mhuni wa makosa ya jinai Richard Mdluli, kimiujiza kulikuwa kumefanikisha kuweka kando ya muunganiko wa serikali kugubikwa na ufisadi, mtakuwa mmekosea.
"Kwa nini mnafikiria Mamlaka ya Uendeshaji wa Mashtaka ya Taifa (NPA) imerejesha mashtaka dhidi ya Jenerali Johan Booysen, mashtaka ambayo tayari yalikuwa yametupwa na mahakama? Lengo ni kumzuia kufanya kazi pamoja na Waziri (wa Polisi Bheki) Cele."
Alisema Booysen "alikuwa na kinyongo kamili akafunua makaratasi yaliyojaa vumbi ya NPA na akatupatia tuchungulie".
"Je, unaweza kufikiri kwamba haya hayakuwa malipo kwa majaribio ya kumfunga Toshan Panday?" Panday ni mfanyabiashara wa Durban aliyehusishwa na rais wa zamani wa Zuma.
Alisema ofisa wa polisi ambaye alijaribu kumhonga Booysen rand milioni mbili (R2m) "fedha taslimu katika mfuko" bado alikuwa kazini.
Kohler-Barnard pia alidai majaribio mawili yalifanywa kutoa uhai wa mwendesha mashtaka mwandamizi baada ya kuwasilisha ripoti ya kurasa 200 kuhusu kwa nini mashtaka dhidi ya Mdluli hayapaswa kufutwa.
"Je, unajua ni nani! Huyo ni waziri wa kivuli wa Sheria Glynnis Breytenbach!" alisema.
"Kuna uthibitisho kutoka vyanzo vitatu vya kujitegemea na vya kuaminika kuwa mavaterani wa MK kutoka Cornubia karibu na Phoenix huko KwaZulu-Natal walichukuliwa kwa ajili ya kufanya kazi hiyo baada ya mikutano na watu si wengine zaidi isipokuwa rais wa zamani aliyeng’atuliwa Jacob Zuma, Super Zuma na Sihle Zikalala. Dudu Myeni pia amehusishwa baada ya kukutana na maveterani hao," alisema Kohler Barnard.