Kinondoni kujenga soko la Sh1bilioni

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta

Muktasari:

  • Akizungumza jijini leo (Alhamisi) katika kikao cha baraza la madiwani, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta alisema   kiasi hicho cha fedha  kinatarajiwa kutengwa kwenye bajeti ya mwaka 2017/2018.

Dar es Salaam. Halmashauri  ya Manispaaa ya Kinondoni imesema itajenga soko  kubwa litakalogharimu Sh 1bilioni katika eneo la Magomeni.

 Akizungumza jijini leo (Alhamisi) katika kikao cha baraza la madiwani, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Benjamin Sitta alisema   kiasi hicho cha fedha       kinatarajiwa kutengwa kwenye bajeti ya mwaka 2017/2018.

Alisema makadirio ya bajeti ya Halmashauri hiyo ambayo ilipitishwa na madiwani ni Sh 160bilioni.