Kura zilizoharibika Bunda Mjini zazua mvutano kortini

Muktasari:

Kesi hiyo imefunguliwa na wakazi wa Bunda ambao wanapinga ushindi wa Ester Bulaya wa Chadema dhidi ya mgombea wa CCM, Stephen Wasira kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita.

Musoma. Aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi wa Jimbo la Bunda Mjini, Lucy Msoffe jana alikuwa kwenye wakati mgumu upande wa wadai ulipombana kutaka maelezo ya idadi halisi ya kura zilizoharibika.

Kesi hiyo imefunguliwa na wakazi wa Bunda ambao wanapinga ushindi wa Ester Bulaya wa Chadema dhidi ya mgombea wa CCM, Stephen Wasira kwenye Uchaguzi Mkuu uliopita.

Jana, msimamizi huyo alidai ni kura 38 pekee ndizo ziliharibika, huku wakili wa waliowasilisha maombi hayo, Hajra Mungula akidai mahakamani kuwa takwimu kutoka ofisi ya msimamizi huyo zinaonyesha zaidi ya kura 100 ziliharibika katika kituo cha Guta pekee.