Lugola atishia kufuta makanisa, misikiti yenye migogoro

Waziri wa Mambo ya Ndani Mh.Kangi  Lugola pamoja na Kanisa la Pendekoste la Leganga, Arumeru,mkoani Arusha akikata ndafu aliyopewa na kanisa hilo alipolitembelea leo Jumapili Julai 29,2018 mkoani Arusha.

Muktasari:

  • Lugola ameagiza masheikh, wachungaji wasishushwe jukwaani

Dar es Salaam. Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema hatasita kufuta makanisa au misikiti inayoshindwa kutatua migogoro ya taasisi hizo.

Ametoa kauli hiyo leo Julai 29, 2018 katika Kanisa la Pentekoste la Leganga, lililopo Arumeru mkoani Arusha.

“Kuanzia sasa, kanisa lolote au msikiti wowote utakaokumbwa na migogoro na kushindwa kuitatua wenyewe; misikiti hiyo, makanisa hayo nitakwenda kuyafuta mara moja,” amesema.

Amesema hatua hiyo inalenga kuhakikisha yanakuwapo makanisa na misikiti inayohubiri amani na utulivu.

Waziri Lugola ameonya askari Polisi wanaowashusha jukwaani masheikh na wachungaji inapofika saa 12:00 jioni, akisema muda huo ukifika waimarishe ulinzi ili waumini wamalize ibada zao vizuri.