Lukuvi kumchukulia hatua aliyempa Makonda shamba

Dar es Salaam. Waziri wa Ardhi,  William Lukuvi amesema atamchukulia hatua mfanyabiashara aliyemkabidhi, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda eneo kwa ajili ya viwanda kwa sababu eneo hilo si lake ni mali ya Serikali.

“Sitaki ardhi itumike kama sehemu ya wafanyabiashara kutakatishia fedha zao chafu,”amesema Lukuvi leo (Jumatatu) katika mkutano na waandishi wa habari.

Lukuvi amesema anataka watu wote wanaomiliki maeneo mijini kujisalimisha kwa maofisa ardhi wa wilaya wa ajili ya uhakiki.