Lwakatare akabidhi mifuko 400 ya saruji aliyoahidi Lowassa

Picha na Phinias Bashaya

Muktasari:

Akikabidhi msaada huo leo, Karumuna amesema kuwa ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Lowassa jana kutokana na uamuzi wa Chadema.

Bukoba. Meya wa Manispaa ya Bukoba, Adronikus Karumuna amemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali (mstaafu), Salum Kijuu mifuko 400 ya saruji iliyoahidiwa na mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa kwa waathirika wa tetemeko la ardhi.

Akikabidhi msaada huo leo, Karumuna amesema kuwa ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Lowassa jana kutokana na uamuzi wa Chadema.

Tukio hilo limeshuhudiwa na Mbunge wa Bukoba Mjini, Wilfred Lwakatare ambaye amesema kwa sasa wananchi wanahitaji msaada na hivyo hakuna sababu ya kuwa na malumbano kwa sababu yoyote.

Jenerali Kijuu ameueleza ujumbe huo kuwa anatumikia wananchi wote kwa usawa bila kuangalia misimamo yao ya vyama na kutoa wito wa wadau wengine kujitokeza kutoa misaada zaidi.