Magufuli ataja jina la kwanza la mtumishi mwenye cheti feki

Rais John Magufuli 

Muktasari:

 Alimtaja mtu huyo kuwa ni Abadallah Polea, ingawa hakueleza ni wa wapi na aliajiriwa katika sekta ipi ya umma.

Dodoma. Rais John Magufuli amekabidhiwa majina ya watumishi wenye vyeti feki na kutaja jina la kwanza la mtu aliyetajwa kwenye ripoti hiyo.

 Alimtaja mtu huyo kuwa ni Abadallah Polea, ingawa hakueleza ni wa wapi na aliajiriwa katika sekta ipi ya umma.

 Amekabidhiwa ripoti hiyo na Waziri wa Utumishi, Angela Kairuki mjini Dodoma leo.