Magufuli atoa siku 60 Tanesco kupeleka umeme kwa Bakhresa

Muktasari:

Rais amesikitishwa na kitendo cha shirika hilo kutochangamkia fursa hasa katika viwanda ambavyo ndio wateja wao wakubwa.

Rais John Magufuli ametoa miezi miwili kwa Shirika la Umeme nchini (Tanesco) kupeleka umeme wa megawati 10 katika kiwanda cha vinywaji baridi cha kampuni ya Bakhresa Products Group kilichopo Mkuranga, Pwani.

Rais amesikitishwa na kitendo cha shirika hilo kutochangamkia fursa hasa katika viwanda ambavyo ndio wateja wao wakubwa.

"Nashindwa kuelewa hvi hawa Tanesco watawezaje kufanya biashara kama hawataki kuwafikia wateja wao. Nataka kufikia Disemba mwaka huu umeme uwe umefika hapa," amesema.

Amelitaka shirika hilo kutambua kipaumbele cha Taifa ambacho ni kuwa ni uchumi wa viwanda. Amesema viwanda vinahitaji umeme wa kutosha kwasababu vinasaidia kuzalisha ajira.