Majambazi yaua askari, yapora silaha usiku huu CRDB Temeke

File Photo

Muktasari:

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alipoulizwa kuhusu tukio hilo, amesema hawezi kuzungumza chochote kwa maelezo kuwa yuko eneo la tukio na amesema atafutwe kesho.

Dar es Salaam. Watu wanaoaminika kuwa ni majambazi usiku huu wamevamia Benki ya CRDB iliyopo Mbande wilayani Temeke mjini hapa na kuua askari kisha kupora silaha na kutokomea kusikojulikana.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro alipoulizwa kuhusu tukio hilo, amesema hawezi kuzungumza chochote kwa maelezo kuwa yuko eneo la tukio na amesema atafutwe kesho.

Uhalifu huo umetokea ikiwa umepita mwaka mmoja tangu kutokea kwa tukio la majambazi kuua askari wanne na kupora silaha baada ya kuvamia kituo cha Polisi Stakishari, Ukonga jijini hapa.