Samia kufunga maadhimisho ya polisi wanawake

Muktasari:

Makamu wa Rais atatembelea mabanda na kukagua shughuli zinazofanywa na polisi wanawake.

Dar es Salaam. Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan ameudhuria maadhimisho ya miaka 10 tangu kuanzishwa mtandao wa polisi wanawake yanayofanyika katika viwanja vya Chuo cha Polisi Kurasini, Dar es Salaam.

Baada ya kuwasili katika maadhimisho hayo yanayofanyika leo Alhamisi Novemba 9,2017, Makamu wa Rais amekagua gwaride maalumu na kupokea maandamano yakiongozwa na farasi na pikipiki.

Maadhimisho yamepambwa na vikundi mbalimbali vya wanawake, vikiwemo vikosi maalumu vya kupambana na uhalifu na cha komandoo wanawake.

Samia pia atatembelea mabanda na kukagua shughuli zinazofanywa na polisi wanawake.

Miongoni mwa  mabanda yaliyopo, lipo kwa ajili ya uchangiaji damu.