Matumaini mapya kodi ya vifungashio vya dawa

Mgeni mwalikwa akisoma kitabu cya hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/2019 ndani ya ukumbi wa Bunge wakati Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alipokuwa akiiwasilisha, jijini Dodoma leo. Picha na Edwin Mjwahuzi

Muktasari:

Anapendekeza kuondolewa kodi ya thamani katika vyakula vya mifugo na dawa za mifugo.

Dodoma. Waziri wa Fedha na Mipango, Philip Mpango  amesema  atapeleka muswada wa sheria kupendekeza kuondolewa kwa kodi katika vifungashio vya  dawa za binadamu zinazotengenezwa na viwanda nchini .

Akizungumza bungeni leo juni 14  Alhamisi jioni hii, wakati akiwasilisha bajeti kuu kwa mwaka wa fedha 2018/19,  Dk Mpango amesema lengo la hatua hiyo ni kuongeza uwekezaji katika sekta ya dawa za binadamu.

Amesema pia anapendekeza kuondolewa kodi ya thamani katika vyakula vya mifugo na dawa za mifugo.