Mbarawa aonya wanaokaa mabondeni

Muktasari:

  • Waziri Mbarawa aliwataka watu hao waliogoma kuhama kuzingatia utabiri wa hali ya hewa juu ya hatari inayowanyemelea

Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Profesa Makame

Mbarawa amewataka watu wanaoishi mabondeni waliogoma kuondoka baada ya

kupata taarifa juu ya hatari inayowanyemelea kuondoka mara moja ili

kuepusha majanga.

Akizungumza leo Machi 23, Mbarawa amesema hivi sasa Mamlaka ya Hali ya

Hewa Nchini (TMA) inatoa taarifa za hali ya hewa inayowataka walioko

katika maeneo ya mabondeni lakini hawako tayari kuondoka.

“Unapopata taarifa ya hali ya hewa kama mahali hapo si lazima maana

yake ni lazima uondoke, vinginevyo utapata shida,”amesema.

Amesema lazima kufuata utabiri wa hali ya hewa ili kujiepusha na

majanga yanayoweza kujitokeza kwa kudharau taarifa zinazotolewa na

mamlaka hiyo.

Amesema zingatia taarifa hali ya hewa ndio kaulimbiu ya

maadhimisho yaliyofanyika jana yakilenga watu kutopuuza utabiri

wa hali ya hewa.

Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk Agnes Kijazi alisema makubaliano ya kimataifa ni kuwa na utabiri wenye usahihi kwa asilimia isiyopungua asilimia 70.

“Utabiri wetu sasa umeongezeka usahihi tumefika hadi asilimia 88

wakati mwingine tunafika asilimia 90,”amesema.

Aidha, amesema wamekuwa wakishirikiana na taasisi nyingine nchini

katika kuchukua hatua wanapotoa taarifa za kutahadharisha watu.