Mbunge amwaga powertiller kila kijiji

Mbunge wa Jimbo la Mbarali, Mbeya, Haroon Pirmohamed (kushoto) akimpa ufafanuzi mkuu wa Mkoa  huo Amosi Makalla (wa pili kushoto) kuhusu matrekta madogo 102 zenye thamani ya zaidi ya Sh500milioni, aliyotoa msaada  kwa kila kijiji cha Wilaya ya Mbarali, ili kuimarisha kilimo. Picha na Godfrey Kahango

Muktasari:

Mbunge wa Mbarali mkoani Mbeya (CCM), Haroon Pirmohamed ametoa msaada wa trekta ndogo za mkono (Powertiller) 102 zenye thamani ya zaidi ya Sh500 milioni ambazo zitagawanywa kwa vijiji vya jimbo hilo. 

Mbarali. Mbunge wa Mbarali mkoani Mbeya (CCM), Haroon Pirmohamed ametoa msaada wa trekta ndogo za mkono (Powertiller) 102 zenye thamani ya zaidi ya Sh500 milioni ambazo zitagawanywa kwa vijiji vya jimbo hilo. 

Mbunge huyo alikabidhi trekita kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla na viongozi wa vijiji 102 vya wilaya hiyo ambao walikabidhiwa na kuondoka nazo.

Pirmohamed alisema wananchi wa jimbo lake ambao wanategemea kilimo wanakabiliwa na changamoto nyingi, hivyo moja ya utatuzi wa changamoto hizo ni trekta hizo hizo kwa kila kijiji ili waweze kuendeshea shughuli zao za kilimo na ujenzi.

“Mimi ni mkulima haswa na wananchi wangu wanategemea kilimo katika uzalishaji wao na wakabiliwa na changamoto nyingi.  Hivyo nimeona kwa kuanzia tu kila kijiji kipatiwe trekta moja ili wazitumie kwenye maendeleo yao.

Ofisa Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika Wilaya ya Mbarali, Yobu Mlomo alimueleza Makalla kwamba 

 msaada huo utafanya wilaya hiyo kuwa na ongezeko la trekta kutoka 2,394 hadi 2,496 ambazo zimesajiliwa.