Mchakato vitambulisho vipya vya Taifa Oktoba 3
Muktasari:
- Katika mchakato huo, wizara hiyo itashirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), ambayo itaratibu mchakato wote wa utambuzi, kuhakiki taarifa za watumishi na kuchukua alama za vidole.
Dar es Salaam. Wizara ya Utumishi na Utawala Bora iliyo chini ya Ofisi ya Rais, imesema kazi ya uhakiki wa watumishi hewa itakwenda sambamba na utoaji wa vitambulisho vipya vya Taifa kwa watumishi wa umma.
Katika mchakato huo, wizara hiyo itashirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), ambayo itaratibu mchakato wote wa utambuzi, kuhakiki taarifa za watumishi na kuchukua alama za vidole.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Angella Kairuki amesema mchakato huo utafanyika kwa wiki mbili kuanzia Oktoba 3 na utawahusisha watumishi wa wizara, taasisi za Serikali zinazojitegemea, tawala za mikoa, mamlaka za Serikali za Mitaa na mashirika ya umma.