Mchungaji Msigwa amjia juu Spika Ndugai kuhusu gharama za Lissu

Muktasari:

  • Spika Ndugai amedai gharama za ndege ya kumpeleka Lissu Nairobi zimelipwa na mbunge wa CCM, Msigwa amesema siyo kweli

Dar es Salaam. Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amemjia juu Spika wa Bunge, Job Ndugai akimtaka kuacha kudanganya kuwa ndege iliyomsafirisha Tundu Lissu ilikodiwa na mbunge wa CCM.

Maelezo ya Mchungaji Msigwa yamekuja saa chache baada ya Spika Ndugai kueleza bungeni kuwa mbunge wa CCM ndiye aliyeagiza ndege kutoka Nairobi kwa gharama za dola za Marekani 9,200 kumsaidia Lissu halafu atakuja kurudishiwa.

Baada ya maelezo hayo Msigwa ambaye yuko na Lissu kwenye matibabu jijini Nairobi ameandika, “Spika Ndugai muogope Mungu, usilete utani katika maisha ya Mh Lissu, umeliongopea Bunge na umma, gharama zote za ndege zimelipwa na Chadema na Watanzania. The parliament deserve better than you!